Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » KAMWE AMJIBU FADLU NA KUSEMA SISI TUNAO WA MARA TATU
    KITAIFA

    KAMWE AMJIBU FADLU NA KUSEMA SISI TUNAO WA MARA TATU

    ChikaoBy ChikaoSeptember 3, 202501 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    KAULI ya Kocha Mkuu wa Simba SC, Fadlu Davids kwamba kikosi chake kinakosa mchezaji mwenye uwezo wa kipekee wa kuamua matokeo ya mechi (maarufu kama X-Factor) imeibua majibu kutoka kwa wapinzani wao wa jadi, Yanga SC.

    Msemaji wa Yanga, Ally Kamwe, hakusita kumjibu Davids kwa tambo akibainisha kuwa ndani ya kikosi cha Wananchi kuna wachezaji kadhaa wenye uwezo huo na zaidi.

    “Hakuna changamoto ya X-Factor ndani ya Yanga. Tuna wachezaji wengi ambao wanaweza kuibadilisha mechi kwa dakika chache tu. Hata baadhi yao tumeongeza kiwango chao cha ubora kiasi kwamba sasa wana X-Factor tatu,” alisema Kamwe.

    Akitaja baadhi ya nyota hao, Kamwe alimtaja Maxi Nzengeli, Clement Mzize na nyota mpya Pacome Zouzoua, akisisitiza kuwa wote ni wachezaji wenye uwezo wa kubeba mchezo mmoja kwa kipaji chao binafsi.

    “Huyu Pacome hata msimu uliopita alithibitisha ubora wake. Lakini kuanzia msimu ujao, kutokana na kiwango chake, atakuwa na X-Factor tatu,” aliongeza Kamwe kwa majigambo.

    Kauli hii inaendeleza mvutano wa maneno kati ya vigogo hao wa soka la Tanzania, jambo linaloongeza ladha ya ushindani kuelekea msimu mpya wa Ligi Kuu Bara.

    Simba SC Yanga SC
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleYANGA KWA SASA NI MWENDO WA “KUPIGA KICHWANI TU”
    Next Article SIMBA YATAMBULISHA CHUMA KIPYA CHA MOTO

    Related Posts

    SIMBA YAANZA USAJILI NA MIPANGO YA UWANJA MPYA BUNJU

    April 8, 2026

    SURE BOY HATIMAE AOMBA KUSEPA YANGA

    April 8, 2026

    HATIMAE MIGUU IMEANZA KUMSALITI CHAMA

    April 7, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    SIMBA YAANZA USAJILI NA MIPANGO YA UWANJA MPYA BUNJU

    SURE BOY HATIMAE AOMBA KUSEPA YANGA

    HATIMAE MIGUU IMEANZA KUMSALITI CHAMA

    AFCON EAST AFRICA TAREHE YATANGAZWA

    MPANZU NA FEI TOTO WAKUTANA USO KWA USO KWENYE VITA YA ASSIST

    IBENGE ATANGAZA VITA JUU YA KIKOSI CHA SIMBA

    MBAPPE: NITACHEZEA TIMU YA TAIFA YA CAMEROON

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.