Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home ยป BAADA YA KUPOTEZA KARIAKOO DABI, SIMBA YATIMKA NCHINI
    KITAIFA

    BAADA YA KUPOTEZA KARIAKOO DABI, SIMBA YATIMKA NCHINI

    ChikaoBy ChikaoSeptember 17, 202501 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    simba
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    KIKOSI cha Simba SC kinachonolewa na Kocha Mkuu, Fadlu Davids asubuhi ya Septemba 17 2025 kimeanza safari ya kuelekea nchini Botswana kwa kupitia nchini Afrika Kusini kwa ajili ya mchezo wa hatua ya awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Gaborone FC.

    Mchezo huo unatarajiwa kupigwa Jumamosi hii Septemba 20 huko Botswana kabla ya wiki moja kurudiana tena kwenye Uwanja wa Mkapa Jijini Dar es Salaam.

    Simba imeondoka leo ikiwa ni saa chache zimeyeyuka tangu watoke kufungwa bao 1-0 katika Kariakoo Dabi dhidi ya Yanga SC Septemba 16 2025 katika mchezo wa Ngao ya Jamii.

    Bao pekee la ushindi kwenye mchezo huo wa ufunguzi wa Ligi Kuu Tanzania Bara inayodhaminiwa na NBC msimu wa 2025/26 limefungwa na Pacome Zouzoua.

    Miongoni mwa wachezaji wa Simba SC ambao wapo kwenye msafara huo ni Moussa Camara, Jonathan Sowah, Joshua Mutale, Seleman Mwalimu, Wilson Nangu.

    Rekodi zinaonyesha kuwa inakuwa ni mara ya sita mfululizo Simba SC kupoteza mbele ya Yanga SC katika mechi za ushindani. Ikumbukwe kwamba msimu wa 2024/25 katika mechi mbili za ligi Simba SC ilifungwa nje ndani.

    Simba SC
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleMOURINHO ATAJWA KUCHUKUA MIKOBA YA KOCHA MKUU WA BENFICA
    Next Article YANGA YAIANZA SAFARI YA ANGOLA BAADA YA KUMCHAPA MTANI

    Related Posts

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.