Author: Chikao

Mwanaume mmoja ameshtakiwa baada ya kukutwa na hatia kutokana na mwanaume mwenye umri wa miaka 46 kutoka Uingereza na Nigeria kuchomwa kisu hadi kufa karibu na uwanja wa Tottenham Hotspur kaskazini mwa London. Okechukwu Iweha alifariki baada ya kuchomwa Kisu huko Haringey, tarehe 7 Aprili 2024, Uchunguzi wa maiti uliofanyika Aprili 10 katika chumba cha kuhifadhi maiti cha Haringey ulitoa sababu ya kifo kama jeraha la kisu kifuani. Mshukiwa, Leandro Kaienga, 28, asiye na makazi maalum, alifikishwa kizuizini katika Mahakama ya Hakimu Willesden mnamo Jumatano, Aprili 24, 2024.Pia ameshtakiwa kwa kupatikana na kitu chenye ncha kali. Polisi wa Metropolitan walimkamata Bw Kaienga mnamo Jumatatu, Aprili 22.

Read More

KATIKA Ligi ya Wanawake Simba Queens imepeta mbele ya Yanga Pricess kwenye Kariakoo Dabi ya Wanawake mchezo uliochezwa Uwanja wa Azam Complex. Baada ya dakika 90 ubao umesoma Yanga Princess 1-3 Simba Queens ambapo pointi tatu zimeelekea kwa Simba Queens. Dakika 45 za mwanzo hakukuwa na mbabe kwa timu zote ambapo ubao ulikuwa unasoma 0-0 mambo yalibadilika kipindi cha pili kwa Simba kupata mabao. Ni Aisha Mnunka huyu alitupia mabao mawili dakika ya 49 na 90 na bao moja ni mali ya Jentrix Shikangwa ilikuwa dakika ya 66. Bao la kufutia machozi kwa Yanga limefungwa na Kaeda Wilson dakika ya 90.

Read More

Shirikisho la Sola Barani Afrika (CAF) limewapa Klab ya RS Berkane ushindi wa Mabao 3 dhidi ya USM Algers ya nchini Algeria. Matokeo haya ni ya mchezo wa Kwanza wa nusu fainali ya Kombe la Shirikisho ambao mchezo huo hakuchezwa kutokana na Sababu za Kidiplomasia na Kisiasa kati ya Algeria na Morocco. Pia CAF imewaagiza USM Algers kwenda Morocco kucheza Mchezo wao wa nusu fainali ya pili dhidi ya RS Berkane na kama hawatafanya hivyo Watafungiwa.

Read More

BAKARI Mwamnyeto nahodha wa Yanga ameweka wazi kuwa moja ya sababu kubwa iliyofanya wakakosa ushindi kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya JKT Tanzania ni sehemu ya kuchezea kutokuwa rafiki. Mchezo wa mzunguko wa pili kati ya JKT Tanzania na Yanga ulichezwa Aprili 24 2024 ambapo awali ulitarajiwa kuchezwa Aprili 23 lakini uliahirishwa kutokana na hali ya hewa ya mvua iliyofanya mpira kushindwa kudunda eneo la kucheza. Baada ya dakika 90 kwenye Uwanja wa Meja Isamuhyo ubao ulisoma JKT Tanzania 0-0 Yanga timu zote mbili ziligawana pointi mojamoja baada ya mchezo kukamilika. Mwamnyeto ameweka wazi kuwa ulikuwa ni mchezo mgumu na wenye ushindani mkubwa hawakuwa na namna kwa kuwa waliambiwa…

Read More

Manchester United wanavutiwa na mshambuliaji wa Brentford na England Ivan Toney na wanaamini kwamba mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 ataleta uzoefu na uongozi kwenye kikosi chao (90min) Hata hivyo, Tottenham wanaweza kumnunua Toney iwapo kutakuwa na ushindani wa kutosha kuipata sahihi yake na kutoa pauni milioni 45. (GivemeSport) Manchester United inalenga kuwaachilia wachezaji 12 msimu huu wa joto, akiwemo fowadi wa Uingereza Marcus Rashford, 26, na kiungo wa kati wa Brazil Casemiro, 32. (Mirror). Mustakabali wa Mauricio Pochettino kama meneja wa Chelsea upo katika mizani na unaweza kutegemea iwapo anaweza kufuzu kwa shindano la Uropa kwa msimu ujao(Times)…

Read More

Familia ya marehemu rapa Tupac ipo kwenye mpango wa kumfungulia mashitaka mwanamuziki Drake baada ya kutumia AI (akili bandia)kutengeneza sauti ya Tupac katika ngoma yake aliyokuwa akimchana Kendrick Lamar. Kwa mujibu wa mwakilishi wa familia ya Tupac, Howard King ameripotiwa kutuma barua kwa Drake afute wimbo huo ndani ya saa 24 endapo hatafanya hivyo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake. Siku tano zilizopita Drake aliachia ngoma iitwayo ‘ Taylor Made Freestyle’ ambapo alitumia AI kutengeneza sauti ya marehemu Tupac na Snoop Dogg, ngoma ambayo ameitoa ikiwa ni dongo kwenda kwa Lamar wimbo huo ukiwa kama ni muendelezo wa bifu lao.…

Read More