Morgan Rogers, mwenye miaka 23, yuko tayari kucheza nje ya England huku mabingwa wa Ulaya Paris Saint-Germain wakiungana na Arsenal, Manchester United na Chelsea katika mbio za kumsajili kiungo mshambuliaji huyo wa Aston Villa. (Talksport)
Manuel Akanji anatarajiwa kuhamia moja kwa moja Inter Milan majira ya joto baada ya klabu hiyo ya Serie A kukubaliana ada ya euro milioni 15 (Β£13m) na Manchester City. (Fabrizio Romano)
Manchester City wanaendelea kujiamini kwamba watamsajili Elliot Anderson kutoka Nottingham Forest kwa dau linaloweza kufikia pauni milioni 100, licha ya ushindani mkubwa. (Sun)
Mshambuliaji wa Italia Lorenzo Lucca atarejea Napoli baada ya mkataba wake wa mkopo kumalizika, huku Nottingham Forest wakikataa kumnunua moja kwa moja. (Corriere dello Sport)
Wakala Jorge Mendes amemuweka sokoni Bernardo Silva wa Manchester City kwa Real Madrid, huku mkataba wake ukimalizika Juni 30. (AS)

Atletico Madrid wameanza mazungumzo na Wolverhampton Wanderers kuhusu kiungo Joao Gomes, lakini huenda wakahitaji takriban pauni milioni 40. (Talksport)
Beki wa Argentina Marcos Senesi amekubaliana kimsingi kujiunga na Tottenham Hotspur kwa uhamisho wa bure akitoka Bournemouth. (Florian Plettenberg)
Manchester United ni miongoni mwa klabu zinazomtaka winga wa AC Milan, Rafael Leao. (Calciomercato)
Kocha wa zamani wa Chelsea, Enzo Maresca, ndiye chaguo la Manchester City endapo Pep Guardiola ataondoka majira ya joto. (Fabrizio Romano)
Juventus wanafikiria kuongeza mkataba wa Pierre Kalulu, lakini Manchester United wanamfuatilia kwa karibu. (Tuttomercatoweb)
Beki wa Uholanzi Micky van de Ven hataki kuongeza mkataba na Tottenham Hotspur na anatafuta kuondoka. (Teamtalk)
