Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » FOLZ ANAJIPANGA KUENDELEZA REKODI YA KUISULUBU SIMBA – KAMWE
    KITAIFA

    FOLZ ANAJIPANGA KUENDELEZA REKODI YA KUISULUBU SIMBA – KAMWE

    ChikaoBy ChikaoSeptember 3, 202502 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    Klabu ya Yanga imesema haifanyi utani kuelekea mchezo wa Ngao ya Jamii, hivyo Kocha Mkuu, Romain Folz, amekuwa na ‘programu’ nne tofauti za maandalizi kuelekea mechi hiyo inayotarajiwa kupigwa, Septemba 16, mwaka huu, katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

    Ofisa Habari wa Klabu hiyo, Ali Kamwe, amesema kocha wa timu hiyo amekuwa na mazoezi ya gym, ufukweni, uwanjani na darasani kwa ajili ya mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Simba ambao utakuwa unaashiria kuanza kwa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu mpya, Septemba 17, mwaka huu.

    Kamwe amesema kocha Romain anataka kuendeleza rekodi za makocha wenzake, Miguel Gamondi na Miloud Hamdi, ambao walikuwa wakiisulubu Simba kila wanapokutana.

    Alisema anataka kuendeleza rekodi ya Yanga kuifunga Simba, ambapo kama atafanikiwa itakuwa ni mara ya sita mfululizo kwa timu yao kuwafunga watani wao wa jadi.

    “Timu inaendelea vizuri kumekuwa na programu tofauti tofauti za uwanjani, gym, ufukweni na darasani, huu ni mwendelezo wa maandalizi hasa kuelekea kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Simba, ingawa tuna mchezo dhidi ya Bandari ya Kenya kwenye kilele cha Wiki ya Mwananchi.

    “Mwalimu ni mpya na wasaidizi wake ni wapya, hilo linakupa picha kwamba wanataka kufanya vizuri. Mwalimu nimemwangalia ana vitu vingi, ana mbinu nyingi sana ambazo zitaanza kuonekana Wiki ya Mwananchi, Ngao ya Jamii na hata kwenye michezo ya kimataifa,” alisema Kamwe.

    Yanga SC
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleRAMOS ALIUMIA SANA KUONDONA MADRID
    Next Article AUDIO Paul Clement – In You MP3 DOWNLOAD

    Related Posts

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.