Wachezaji wa Manchester City watakuwa na siku tatu nje ya uwanja ili kufurahia likizo ya Krismasi lakini meneja Pep Guardiola anasema yeyote atakayefanya makosa ya kiwango cha juu wakati wa kurudi kwao hatacheza dhidi ya Nottingham Forest Jumamosi.
“Kila mchezaji ana uzito. Wanarudi tarehe 25 na nitakuwepo kudhibiti ni kilo ngapi zinazoongezeka, (ili kuona kama) zina mafuta,” alisema Guardiola, ambaye anajulikana kwa kuwa mkali kuhusu lishe na urekebishaji.
Mara tu wanapofika baada ya siku tatu nataka kuona watakavyorudi. Wanaweza kula lakini nataka kuwadhibiti. Lazima nifanye uteuzi wa (Desemba) 27 dhidi ya Nottingham Forest.
Hebu fikiria mchezaji mmoja na sasa yuko kamili lakini atawasili na kilo tatu zaidi. Atabaki Manchester, Hatasafiri kwenda Nottingham Forest.
City, ambao walishinda West Ham United 3-0 mwishoni mwa jumalilopita, wako nyuma kwa pointi mbili dhidi ya vinara Arsenal baada ya michezo 17.










Leave a Reply