Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » ALI KAMWE: SIMBA YA SAFARI HII NI MBOVU SANA
    KITAIFA

    ALI KAMWE: SIMBA YA SAFARI HII NI MBOVU SANA

    ChikaoBy ChikaoSeptember 18, 202502 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    Ali Kamwe, Ofisa Habari wa Yanga SC amesema kuwa Simba SC ya msimu huu wa 2025/26  ni mbovu kuliko ile ya msimu uliopita wa 2024/25.

    Yanga SC kwa sasa mkononi wana taji la Ngao ya Jamii walitwaa kwa kushinda mbele ya Simba SC mchezo uliochezwa Uwanja wa Mkapa, Septemba 16 2025 ikiwa ni mchezo wa ufunguzi wa msimu mpya wa 2025/26..

    Baada ya dakika 90 ubao wa Uwanja wa Mkapa ulisoma Yanga SC 1-0 Simba SC, bao la ushindi likifungwa na Pacome dakika ya 53 akiwa ndani ya 18 alipomtungua Moussa Camara kipa namba moja wa Simba SC.

    Kamwe amesema: “Simba ya msimu huu ni mbovu zaidi kuliko ya msimu uliopita, ni mbovu kwa sababu wachezaji wapya hawana ubora wa kushindana naona wanapambana kutafuta matokeo uwanjani.

    “Kwa hali ilivyo ninaona kabisa ndoto yangu ya kufikisha furaha ya kumfunga Simba SC mara kumi mfululizo nazidi kuiona na kutwaa ubingwa wa ligi kwa mara nyingine tena,”alisema Kamwe.

    Kikosi cha Yanga SC kwa sasa kipo nchini Angola ambapo kipo hapo kwa ajili ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika ikiwa ni hatua ya awali.

    Yanga Ijumaa hii ya Septemba 19 watakuwa Uwanja wa Estadio 11 de Novembro wakicheza na Wiliete Sports Clube mechi ya awali Ligi ya Mabingwa Afrika.

    Mchezo huu unatarajiwa kuchezwa kuanzia saa 12:00 jioni ambapo Watanzania na dunia itashuhudia burudani hiyo  mubashara kupitia AzamSports1HD.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleHII HAPA RATIBA YA ANGA LA KIMATAIFA, AZAM FC, SIMBA, YANGA SC, SINGIDA BS
    Next Article SINGIDA BS YAANZA MAZOEZI YA KWANZA KIGALI, RWANDA

    Related Posts

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.