Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » CLEMENT MZIZE BADO ANA MKATABA NA YANGA
    KITAIFA

    CLEMENT MZIZE BADO ANA MKATABA NA YANGA

    ChikaoBy ChikaoAugust 18, 202501 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Yanga
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    MSHAMBULIAJI namba moja kwa wazawa wenye mabao mengi msimu wa 2024/25 Clement Mzize bado ana mkataba na Yanga SC kuelekea msimu wa 2025/26.

    Mzize amekuwa akitajwa kuwa katika rada za timu mbalimbali ambapo kuna timu moja kutoka Tunisia inatajwa kuweka dau kubwa mezani kupata saini yake kwa ajili ya changamoto mpya.

    Rekodi zinaonyesha kuwa msimu wa 2024/25 Mzize alifunga jumla ya mabao 14 kwenye ligi ambapo Yanga SC walitwaa ubingwa na safu ya ushambuliaji ya timu hiyo ilifunga jumla ya mabao 83 ikiwa ni timu iliyofunga mabao mengi.

    Ali Kamwe, Ofisa Habari wa Yanga SC amebainisha kuwa Mzize ni mchezaji wa Yanga SC na kuna ofa ambazo zipo ikiwa zitajibiwa taarifa itatolewa kuhusu mchezaji huyo.

    “Clement Mzize bado ana mkataba na Yanga SC hivyo kwa sasa ni mali yetu mashabiki ninapenda kuwahakikishia kuwa mchezaji tupo naye hajaondoka. Kuhusu ofa kuna ofa zaidi ya mbili kwa mchezaji wetu hizo zinafanyiwa kazi.

    “Makubaliano yakifika taarifa itatolewa kwa kuwa mchezaji bado yupo hivyo hakuna tatizo kuhusu wengine kusema hivi na vile, viongozi tupo na masuala ya kimkataba yanatatuliwa kwa mkataba.”

    Yanga SC
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleMOROCCO KUKUTANA NA MOROCCO, KIVUMBI CHAN 2024
    Next Article SIMBA YACHEZEA MABAO 4 HUKO MISRI KWENYE MCHEZO WA KIRAFIKI

    Related Posts

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.