GWIJI wa Ligi Kuu England, Wayne Rooney, ameonya kuwa Mikel Arteta anaweza kufukuzwa kazi endapo atashindwa kuipa Arsenal taji la Ligi Kuu msimu huu 😳🏆
Arsenal kwa sasa inaongoza ligi kwa pointi sita mbele ya Manchester City, na imekuwa vinara wa kubashiriwa kushinda taji lao la kwanza tangu mwaka 2004. Kwa mujibu wa Rooney, nafasi hiyo nzuri inaondoa kabisa visingizio kwa Arteta.
Akizungumza kwenye kipindi cha The Wayne Rooney Show, amesema: “Arsenal wamemuunga mkono Arteta kwa kiwango kikubwa na wamempa kikosi bora sana. Kama hawatashinda mwaka huu, kutakuwa na presha kubwa kwake, bila shaka.”
Rooney pia anaamini ushindi wa kusisimua wa Man City dhidi ya Liverpool Anfield unaweza kuwa umeathiri kisaikolojia kikosi cha Arteta. City ilirejea kutoka nyuma na kushinda 2-1, hali iliyopunguza pengo kutoka pointi tisa hadi sita.
Je, Arteta atakamilisha kazi au presha itamlemea?