LUIS DIAZ yupo kiwango bora cha maisha yake akiwa na Bayern Munich hii ni ‘material’ ya Ballond’or kabisa, tangu atue kwa wabishi hao wa soka la Ujerumani amekuwa nyota muhimu mno kwenye kikosi hicho.
Hadi sasa amehusika kwenye mabao 30 ndani ya michezo 30 aliyoiwakilisha nembo ya mabosi zake.
Kama Bayern Munich watashinda mataji makubwa na timu yake ya taifa ya Colombia ikafanya vizuri kwenye Kombe la Dunia basi huenda tukazungumza mengine kwenye Ballon d’or mwaka huu.