Klabu ya Yanga, imetangaza kumrejesha kocha Abdihamid Moalin kuwa kocha Msaidizi chini ya Kocha Mkuu Pedro Gonçalves hatua ambayo klabu hiyo imeeleza kuwa imalenga kutatua changamoto ya kiufundi klabu hiyo inayopelekea kupata wakati mgumu kupata matokeo mazuri na kucheza vizuri.
Taarifa ya Machi 23, 2026 iliyotolewa na klabu hiyo na klabu hiyo baada ya kikao cha kufanya tathimini ya timu hiyo baada ya kumalizika kwa mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu msimu huu imeeleza kuwa uongozi WA klabu umegundua uwepo wa changamoto ya kiufundi inayoifanya Timu icheze aina tofauti ya uchezaji (style of play) ile ambayo imezoelekea na kuendana na wachezaji walio ndani ya kikosi.
