Home KITAIFA YANGA SC WAPO KAZINI, KUMSHUSHA WINGA WA KAZI

YANGA SC WAPO KAZINI, KUMSHUSHA WINGA WA KAZI

224
0

KLABU ya Yanga ipo katika mazungumzo ya mwishoni katika kuipata saini ya winga wa Singida Black Stars, Edmund John ili awe sehemu ya kikosi hicho katika msimu ujao.

Inadaiwa makubaliano binafsi kati ya mchezaji na Yanga tayari yamekamilika na mchezaji yupo tayari. Nyota huyo alikuwa tishio katika mchezo wa Nusu Fainali wa Kombe la CRDB dhidi ya Simba.

Yanga wamempatia mkataba wa miaka mitatu winga huyo, kilichobakia makubaliano kati ya Yanga na Singida Black Stars yapo hatua za mwishoni kukamilika ili nyota huyo asaini.

Advertisement

Tayari Yanga SC ipo kambini kwa maandalizi ya msimu mpya wa 2025/26 wakiwa kwenye mazoezi ya awali kuelekea msimu mpya.

Yanga SC ni mabingwa watetezi kwa msimu ujao baada ya kutwaa taji msimu wa 2024/25 wakiwa na pointi 82 baada ya mechi 30.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here