KITAIFA

AUGUST HII, SIMBA KUKIPIGA NA ‘APR’ YA KUTOKA RWANDA?

Klabu ya Simba imeripotiwa kupokea mwaliko kutoka nchini Rwanda wa klabu ya APR kucheza mechi ya kirafiki.

APR ambayo itaiwakilisha Rwanda kwenye michuano ya ligi ya mabingwa (CAF CL) msimu ujao, imeomba kujipima na Simba katika mchezo ambao umepangwa kupigwa kati ya August 1 na August 03

Bado Simba haijathibitisha kushiriki mchezo huo kwani itategemea na mipango yake ya Pre-Season

Endapo Simba itaweka kambi yake ya Pre-Season nje ya Tanzania huenda ikashindwa kushiriki mchezo huo katika tarehe iliyopangwa

Kulingana na taarifa za awali, kikosi cha Simba kinatarajiwa kuanza maandalizi ya pre-season Julai 25, siku ya Ijumaa.

Leave a Comment