Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » SIMBA YAKATAA UHUNI KWENI KWENYE MPIRA WA MIGUU
    KITAIFA

    SIMBA YAKATAA UHUNI KWENI KWENYE MPIRA WA MIGUU

    ChikaoBy ChikaoOctober 14, 202502 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    simba
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    UONGOZI wa Simba SC umeweka wazi kuwa haukubaliani na vitendo vya kihuni kwenye mpira wa miguu kwa kuwa unarudisha nyuma maendeleo ya wachezaji na timu kiujumla.

    Simba SC inapeperusha bendera katika Ligi ya Mabingwa Afrika ikiwa hatua ya pili inatarajiwa kucheza mchezo wake wa kimataifa dhidi ya Nsiginzini Hotspurs Oktoba 19 2025 pia inaongoza ligi ikiwa na pointi sita baada ya mechi mbili.

    Ahmed Ally, Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba SC amesema kuwa vitendo vya kihuni ambavyo vinatokea uwanjani kwa wachezaji kuchezeana rafu mbaya vinaumiza wachezaji na kudumaza maendeleo ya mpira kutokana na wachezaji kukaa nje muda mrefu wakipambania hali zao.

    “Vitendo vya kihuni kwenye mpira wa miguu havifai kwa kuwa vinadumaza maendeleo ya mpira na sio mpira tu hata maendeleo ya mchezaji husika yanadumaa kwa kuwa maisha yake yapo kwenye mpira hapo anaendeleza maisha na familia.

    “Inapotokea mchezaji mwingine anamchezea faulo mbaya mchezaji hii inamaana kwamba anahatarisha maisha yake na maisha ya familia yake. Wapo wachezaji ambao wamekuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu na hii imetokana na kufanyiwa vitendo vya kihuni.

    “Muhimu kila mchezaji kuwa mlinzi wa mchezaji mwengine hili litafanya mpira usiwe wa kihuni na rafu mbaya hazifai kwa kuwa mpira ni maisha na maisha yanatengenezwa kila hatua ambayo inapigwa.”

    Simba SC
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleSIMBA YAENDELEZA KAMPENI YA KUTOKOMEZA JEZI FEKI
    Next Article KOMBE LA DUNIA 2034 KUCHEZWA JANUARY 2035

    Related Posts

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.