Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » HIVI HAPA VIINGILIO MECHI YA MARUDIANO SIMBA VS NSINGIZINI
    KITAIFA

    HIVI HAPA VIINGILIO MECHI YA MARUDIANO SIMBA VS NSINGIZINI

    ChikaoBy ChikaoOctober 23, 202501 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    simba
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    Simba SC vs Nsingizini Hotspurs CAF Champions Oktoba 26,2025 unatarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa ikiwa ni mchezo wa maamuzi.

    Ipo wazi kwamba katika mchezo wa kwanza uliochezwa Oktoba 19 2025 Eswatini, Simba SC iliibuka na ushindi wa mabao 3-0.

    Kwenye mchezo huo wa ugenini, Kibu Dennis alifunga mabao mawili na bao la ufunguzi lilifungwa na beki wa kati Wilson Nangu kwa pigo la kichwa akimalizia kona ya Maema.

    Ahmed Ally, Meneje wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba SC ameweka wazi kuwa huo ni mchezo muhimu na Wanasimba wanapaswa kujitokeza kwa wingi.

    “Kuelekea mchezo huu tumeweka viingilio vya kitajiri. Viingilio ni Tanzanite – Tsh. 250,000, Platinum – Tsh. 150,000, VIP A – Tsh. 30,000, VIP B – Tsh. 20,000, VIP C – Tsh. 10,000 na Mzunguko – Tsh. 5,000.

    “Tunaamini kwamba hakuna Mwanasimba ambaye atashindwa kutoa 5,000 kushuhudia burudani kutoka kwa wachezaji wake wenye uwezo na kupata burudani. Njooni kwa wingi huu ni mtoko usije peke yako njoo na familia yako ufurahie kuipelekea Simba yako hatua ya makundi,”.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleRonaldo kumsogeza Lewandowski Al-Nassr
    Next Article ARNE SLOT APOTEZA MECHI NNE MFULULIZO LIVERPOOL

    Related Posts

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.