Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » MOURINHO ATANGAZA VITA KALI DHIDI YA CHELSEA LEO
    KIMATAIFA

    MOURINHO ATANGAZA VITA KALI DHIDI YA CHELSEA LEO

    ChikaoBy ChikaoSeptember 30, 202501 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    Kocha Mkuu wa Benfica ya Ureno, Jose Mourinho, anarejea leo kwenye dimba la Stamford Bridge, uwanja wenye historia kubwa katika maisha yake ya soka. Safari hii anarejea kama mpinzani, akiiongoza Benfica kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya mabingwa wa dunia, Chelsea. Mourinho alitangazwa kuwa kocha mkuu wa Benfica wiki iliyopita na leo anakabiliwa na mtihani wake mkubwa wa kwanza akiwa na timu hiyo mpya.

    Akizungumza kuelekea mchezo huo, Mourinho alisema anajihisi kama yupo nyumbani lakini sasa anawakilisha Benfica na lengo lake ni moja tu — kushinda. “Najihisi kama niko nyumbani, lakini ndani ya dakika 90 sitafikiria nilikotoka. Mimi si ‘The Blues’ tena, mimi ni mwekundu wa Benfica na nataka kushinda,” alisema.

    Mourinho aliwahi kuinoa Chelsea katika vipindi viwili tofauti (2004–2007 na 2013–2015) na kuandika historia kwa kutwaa mataji makubwa ikiwemo ubingwa wa Ligi Kuu England mara tatu, Kombe la FA mara moja, Kombe la Ligi mara tatu na Ngao ya Jamii mara moja. Kurejea kwake Stamford Bridge leo ni tukio la kihistoria linaloleta kumbukumbu nyingi, huku dunia ya soka ikisubiri kuona kama “The Special One” ataandika ukurasa mwingine wa kukumbukwa.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleWAJUE WAPINZANI WA SIMBA MECHI INAYOFUATA CAF
    Next Article TETESI: NABI YUPO MBIONI KUIONA KLABU HII KUBWA NCHINI

    Related Posts

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    March 24, 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    March 20, 2026

    RICHARLISON SHUJAA WA TOTTENHAM VS LIVERPOOL, WAIPINGIZA MAKALI

    March 16, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.