BAADA ya kiungo mshambuliaji wa Yanga SC Aziz Ki taarifa kueleza kuwa anaondoka ndani ya kikosi hicho kuelekea Wydad inaelezwa kuwa kuna nyota mwingine tena anaondoka katika kikosi hicho.
Aziz Ki amekuwa kwenye mwendo mzuri ndani ya Yanga SC akiwa kacheza jumla ya mechi 114 na kutoa pasi 57 za mabao huku akifunga jumla ya mabao 32.
Ni Clement Mzize chaguo la kwanza la Kocha Mkuu, Miloud Hamdi anatajwa kuwa kwenye hesabu za mabosi wa Zamalek ambao wanahitaji kupata huduma yake.
Mshambuliaji huyo kafunga jumla ya mabao 13 kwa msimu wa 2024 kwenye ligi akiwa ni mzawa namba moja mwenye mabao mengi.
Mbali na Zamalek inaelezwa kuwa mabosi wa Kaizer Chiefs wanahitaji huduma ya mshambuliaji huyo ambaye mguu wakwe wenye nguvu ni ule wa kulia na bao lake la kwanza msimu wa 2024/25 alifunga mbele ya Kagera Sugar, Uwanja Kaitaba ambapo alianzie benchi kwenye mchezo huo.
Alipachika bao la pili akitumia pasi ya kiungo mshambuliaji Aziz Ki baada ya dakika 90 ubao ukasoma Kagera Sugar 0-2 Yanga SC.