Naibu Spika wa Bunge, Mussa Azzan Zungu katika bunge jana Tarehe 24, May alikumbusha bunge hilo kuwa Jumapili ya leo kuna jambo muhimu la kitaifa.
Akizungumza wakati akihitimisha shuguli za bunge, Zungu amesema historia inakwenda kuandikwa siku ya Jumapili.
Ifahamike kwamba Jumapili kikosi cha Simba kitacheza fainali ya pili ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya RS Berkane ya Morocco.
Mchezo wa kwanza Simba ilipoteza 2-0, lakini wanaamini watapindua meza na kutwaa ubingwa siku ya leo Jumapili visiwani Zanzibar.