Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home ยป NYOTA WA FOUNTAIN GATE ALAMBA MKATABA WA MIAKA 17
    KITAIFA

    NYOTA WA FOUNTAIN GATE ALAMBA MKATABA WA MIAKA 17

    ChikaoBy ChikaoJuly 27, 202501 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    TIMU ya Fountain Gate FC imemtambulisha mchezaji chipukizi Juma Issa Abushiri (Chuga) kutoka timu ya taifa ya vijana ya Tanzania (U-17). Nyota huyo amesaini mkataba wa miaka mitano kuwa kwenye timu hiyo ambayo ina uhakika wa kushiriki Ligi Kuu Tanzania Bara ya NBC ambayo ni namba nne kwa ubora msimu wa 2025/26.

    Akizungumza katika Hoteli ya Tanga Beach Resort jijini Tanga, baada ya kumsainisha mchezaji huyo, Rais wa Fountain Gate, Japhet Makau, amesema kuwa usajili huo ni sehemu ya kuendeleza utamaduni wa timu hiyo wa kuwapa nafasi vijana.

    Ameeleza kuwa Juma Issa ni zao la timu za vijana za Fountain Gate tangu akiwa mdogo, na alisoma katika shule za timu hiyo, ambako kipaji chake kiligunduliwa.

    Amesema kuwa lengo la kuwasajili vijana ni kuwapa fursa ya kuonesha ushindani katika Ligi Kuu na kufungua milango ya kucheza soka nje ya nchi.

    Aidha, katika msimu uliopita, timu hiyo ilipandisha vijana takriban wanane walio chini ya umri wa miaka 20, ambao wamepata nafasi ya kuonesha uwezo wao katika timu ya wakubwa.

    Ofisa Habari wa Fountain Gate, Issa Mbuzi ameweka wazi kuwa mpango mkubwa wa timu hiyo ni kufanya vizuri kwa msimu mpya na timu ambazo ziliwafunga hazitawafunga msimu mpya wa 2025/26.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleUSAJILI WA KWANZA SIMBA HUU HAPA, MSHAMBULIAJI WA MABAO KUTAMBULISHWA
    Next Article KIVUMBI LEO FAINALI YA WAFCON NIGERIA VS MOROCCO

    Related Posts

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.