Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home ยป MOHAMED HUSSEIN AFICHUA VITA YAKE NA BOKA INAYOENDELEA YANGA
    KITAIFA

    MOHAMED HUSSEIN AFICHUA VITA YAKE NA BOKA INAYOENDELEA YANGA

    ChikaoBy ChikaoSeptember 24, 202502 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    MOHAMED HUSSEIN
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    Beki mpya wa Yanga, Mohamed Hussein ‘Tshabalala’, amefunguka kuwa ni kweli kuna ushindani mkali wa namba kati yake na Chadrack Boka, lakini pia akieleza hadhani kama atakuwa anaanzia benchi mechi zote kwani kuna mashindano mengi sana mbele yao.

    Tshabalala, aliyejiunga na Yanga msimu huu akitokea Simba, amebainisha kuwa kwenye kikosi chote cha Yanga kuna ushindano mkali wa namba kwenye idara zote na si eneo analocheza yeye, hivyo Kocha Mkuu, Romain Folz, ndiye atakayekuwa akiamua nani anaanza na nani aingie baadaye.

    Beki huyo wa kushoto, alisema hayo kutokana na kuonekana akianzia benchi kwenye mechi tatu ambazo Yanga imecheza mpaka sasa.
    “Mwalimu ndiye atakuwa anachagua nani aanze nani amalize, timu hii imekamilika kila idara, ina wachezaji bora zaidi ya mmoja na yeyote anayeanza timu inapata ushindi.

    “Kwa maana hiyo ni kwamba kweli kuna ushindani wa namba, lakini si kila siku atakayeanza basi atakuwa anaanza mechi zote, mashindano yako mengi sana, naamini kila mtu atapata nafasi ya kuanza na kucheza mechi nyingi kadri iwezekanavyo,” alisema beki huyo wa kushoto ambaye pia huichezea Timu ya Taifa Stars.

    Katika mechi ya kilele cha Wiki ya Mwananchi dhidi ya Bandari ya Kenya, Ngao ya Jamii dhidi ya Simba na mchezo wa kwanza hatua za awali, Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Wiliete de Benguela ya Angola, mchezaji huyo ambaye pia hutumia jina la Zimbwe Jr, zote hizo aliingia kipindi cha pili kama mchezaji wa akiba, hivyo kuzua minong’ono kwa baadhi ya mashabiki kuwa amekuwa mchezaji wa akiba, badala ya kuanza michezo yote kama alivyokuwa Simba.

    Yanga SC
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleEDO KUMWEMBE: SIJAONA CHOCHOTE KWA KOCHA FADLU
    Next Article SERIKALI YATOA KAULI JUU YA SAKATA LA PAMBA JIJI KUFANYA MAZOEZI GIZANI

    Related Posts

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.