Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » EDO KUMWEMBE: SIJAONA CHOCHOTE KWA KOCHA FADLU
    KITAIFA

    EDO KUMWEMBE: SIJAONA CHOCHOTE KWA KOCHA FADLU

    ChikaoBy ChikaoSeptember 24, 202502 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Fadlu
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    Sidhani kama Simba wana kitu kikubwa cha kupoteza katika hili. Kuna kocha huwa anawaweka katika wakati mgumu akiamua kuondoka zake. Kuna aina ya mpira anaweza kuondoka nayo. Hadi sasa hatutajua mpira wa Fadlu ni upi hasa. Kuanzia pale alipoishika timu na mpaka pale alipokwenda likizo kisha akarudi, akahusika katika usajili na kisha kwenda na timu kambini Misri.

    Wakati ikiwa pale Ismailia chini ya Fadlu sidhani kama Simba imetengeneza aina yoyote ya mpira wa kushtua chini ya Fadlu. Siku hizi makocha wanatengeneza falsafa zao. Unaweza kuchagua kuwa bora katika kushambulia, au kukaa na mpira, au kujihami. Sijaona LOLOTE ambalo Fadlu amelitengeneza kwa ufasaha wakati timu ikiwa kambini kule Misri.

    Tukianzia mechi ya Gor Mahia katika siku ya Simba Day. Wageni waliwafundisha wenyeji namna ya kukaa na mpira kwa muda mrefu. Bahati mbaya tu wageni waliruhusu mabao mawili. Halafu likaja pambano la Simba na Yanga. Simba walionekana kucheza vizuri. Sio kwamba walikuwa wazuri, hapana, ni vile tu Yanga walitarajiwa kuwa wazuri zaidi ya Simba lakini hawakucheza katika kiwango chao. Bado mwisho wa yote Fadlu aliendelea kuweka rekodi ya kupoteza pambano jingine la Dabi dhidi ya mtani kitu ambacho kimekuwa cha kawaida kwake.

    Na Jumamosi jioni Simba ilikuwa Gaborone ikicheza pambano la kimataifa la ushindani dhidi ya Gaborone United Simba haikuonyesha kama ilikuwa kambini Misri ikipika kitu. Ilicheza ovyo ingawa ilishinda 1-0. Sijakutana na shabiki wa Simba aliyeridhika na kiwango cha timu

    Kama akiondoka sasa Simba watakuwa katika nafasi nzuri ya kuanza na kocha mpya kabla msimu haujachanganya. Labda wachezaji watamuelewa mapema kocha mpya wakati msimu angali ukiwa mchanga.”

    — Legend, Edo Kumwembe. [JichoLaMwewe]

    Simba SC
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleHAYA HAPA MAGAZETI YA LEO SEPTEMBA 24, 2025
    Next Article MOHAMED HUSSEIN AFICHUA VITA YAKE NA BOKA INAYOENDELEA YANGA

    Related Posts

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.