Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » ENG. HERSI SAID AENDELEA KUIBEBA SOKA LA AFRIKA KUPITIA ACA
    KITAIFA

    ENG. HERSI SAID AENDELEA KUIBEBA SOKA LA AFRIKA KUPITIA ACA

    ChikaoBy ChikaoJuly 6, 202501 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Hersi
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    Mwaka uliopita, Chama cha Umoja wa Vilabu Afrika (ACA) chini ya uongozi wa Eng. Hersi Said, kilifanikiwa kushawishi CAF kutoa dola 50,000 kwa kila klabu iliyoshiriki Ligi ya Mabingwa Afrika (CAF CL) na Kombe la Shirikisho (CAF CC) katika hatua ya awali.

    Kwa msimu huu mpya, ACA imeendelea kupigania maslahi ya vilabu barani Afrika kwa mafanikio zaidi. Kupitia mazungumzo na ushawishi wao kwa CAF, imeidhinishwa kuwa klabu zitakazoshiriki hatua ya awali ya CAF CL na CAF CC zitalipwa dola 100,000 kila moja kwa ajili ya maandalizi.

    Ikumbukwe, kabla ya uwepo wa ACA, klabu shiriki katika hatua za awali za mashindano hayo hazikuwa zikipewa msaada wowote wa kifedha na CAF.

    Hatua hii imepongezwa na wadau wengi wa soka barani Afrika kama ishara ya kweli ya mapambano ya kuleta usawa na maendeleo ya vilabu vya Afrika vilivyo katika mazingira magumu ya kifedha.

    Kwa mara nyingine tena, Eng. Hersi Said ameendelea kuthibitisha kujitolea kwake kwa dhati katika kuendeleza soka la Afrika na kupigania maslahi ya vilabu.

    “Hersi anazidi kuipambania football ya Afrika.” – @alikamwe

    Yanga SC
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleALI KAMWE, ASHANGAZWA NA MAUNO YA BONGE LA DADA
    Next Article BERNARD MORRISON ATOA SHUKRANI KWA WALIOSIMAMA NAYE KATIKA SAFARI YA KUPONA MAJERAHA YA GOTI

    Related Posts

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.