Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home ยป WAZIRI AWESO AWAKILISHA WAZIRI MKUU KATIKA KILELE CHA SIMBA DAY 2025
    KITAIFA

    WAZIRI AWESO AWAKILISHA WAZIRI MKUU KATIKA KILELE CHA SIMBA DAY 2025

    ChikaoBy ChikaoSeptember 10, 202501 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    simba
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    Waziri wa Maji, Jumaa Hamidu Aweso, amewasili katika Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam akimuwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, kama Mgeni Rasmi katika kilele cha Wiki ya Simba (Simba Day 2025).

    Katika tukio hilo kubwa linaloendelea hivi sasa, Waziri Aweso ameungana na viongozi wa Simba SC pamoja na maelfu ya mashabiki waliomiminika kushuhudia burudani, utambulisho wa kikosi kipya cha msimu huu na shamrashamra zinazotambulisha heshima na hadhi ya klabu hiyo.

    Simba Day, ambayo imekuwa ikifanyika kila mwaka, ni sehemu ya utamaduni wa klabu hiyo kongwe barani Afrika, ikileta pamoja wapenzi wa soka na burudani huku ikitoa taswira ya mshikamano mkubwa kati ya klabu na mashabiki wake.

    Kilele cha maadhimisho ya mwaka huu kimeambatana na burudani kutoka kwa wasanii wakubwa, pamoja na matarajio makubwa ya mashabiki kuhusu kikosi kipya cha Simba kitakachoingia dimbani kwenye michuano ya ndani na kimataifa msimu wa 2025/26.

    Simba SC
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleRASMI DEPAY AFIKIA REKODI YA VAN PERSIE UHOLANZI
    Next Article ALI KAMWE AMETOA AHADI HII YANGA DAY 2025

    Related Posts

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.