Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » YANGA SC YAZITAKA TATU ZA TANZANIA PRISONS
    KITAIFA

    YANGA SC YAZITAKA TATU ZA TANZANIA PRISONS

    ChikaoBy ChikaoJune 18, 202501 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    KOCHA Mkuu wa Yanga SC, Miloud Hamdi amesema kuelekea kwenye mchezo wao wa mzunguko wa pili dhidi ya Tanzania Prisons msimu wa 2024/25 ambacho wanahitaji ni pointi tatu muhimu ndani ya dakika 90.

    Yanga SC itakaribishwa na Tanzania Prisons kwenye mchezo wa ligi unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Sokoine, Juni 18 2025 saa 10:00 ikiwa ni mzunguko wa pili.

    Miloud amesema:”Tunawaheshimu sana Tanzania Prisons, lakini sisi ni Yanga. Nina wachezaji wenye uzoefu na uwezo mkubwa. Tunajua utakuwa mchezo mgumu lakini hatuna sababu ya kuwaza sana kuhusu hilo. Tumekuja kushindana kwa tahadhari kubwa na ambacho tunahitaji ni pointi tatu muhimu.”

    “Tumekuja Mbeya kusaka alama tatu tunawashukuru sana mashabiki, nimefanya kazi Klabu mbalimbali kubwa lakini mashabiki wa Yanga ni mashabiki wa mfano. Naamini kesho kwa mchango wao Uwanjani basi tutakuwa na wakati mzuri. Niwaombe sana mashabiki wajitokeze kwa wingi”

    Kwenye msimamo Yanga SC ni nafasi ya kwanza ikiwa na pointi 73 baada ya mechi 27 inakutana na Tanzania Prisons iliyo nafasi ya 13 na pointi 30 baada ya mechi 28.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleKISA KUMPIGA MWAMUZI, ‘KIHIMBWA’ ASIMAMISHWA FOUNTAIN GATE FC
    Next Article KENGOLD VS SIMBA SC HESABU KALI ZINAPIGWA

    Related Posts

    KOCHA WA YANGA HAELEWI, VIONGOZI WABADILISHA UELEKEO

    March 25, 2026

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    TETESI: TIMU YA MESSI YAMFUKUZIA BERNARDO SILVA

    KOCHA WA YANGA HAELEWI, VIONGOZI WABADILISHA UELEKEO

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.