Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » FEISAL SALUM AFICHUA HESABU ZA TANZANIA CHAN 2024
    KITAIFA

    FEISAL SALUM AFICHUA HESABU ZA TANZANIA CHAN 2024

    ChikaoBy ChikaoAugust 20, 202501 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    WAKATI Tanzania Agosti 16 2025 kwenye mchezo wa CHAN 2024 ikishuhudia ubao wa Uwanja wa Mkapa ukisoma Afrika ya Kati 0-0 Tanzania, kiungo Feisal Salum amebainisha kuwa watapambana katika hatua ya robo fainali kupata matokeo mazuri.

    Mchezo huo uliopita hatua ya makundi ulikuwa wa kwanza kwa Tanzania kugawaa pointi mojamoja. Katika mechi tatu ambazo zilipita za makundi Tanzania ilishinda zote ikikusanya pointi 9.

    Baada ya mechi nne, Tanzania inaongoza kundi B ikiwa na pointi 10 itacheza na Morocco hatua ya robo fainali mchezo unaotarajiwa kuchezwa Agosti 22, 2025 Uwanja wa Mkapa.

    Nyota huyo ambaye alichaguliwa kuwa mchezaji bora baada ya mchezo alibainisha kuwa wanatambua kuna kazi kubwa mbele yao hivyo watapambana kuwa bora zaidi.

    “Kwenye mchezo wetu uliopita haikuwa shida katika kutafuta matokeo kwa kuwa tulienda na game plan yetu ya kile ambacho tulifundishwa mazoezini. Ambacho walifanya wapinzani wetu ni kuziba nafasi ambazo tulizifanyia mazoezi. Mimi mchezaji katika matokeo tuliyopata hatujaridhika.

    “Tulitegemea matokeo kwenye mchezo wetu. Wenzetu walituheshimu na kuja kwa umakini. Mchezo huu umepita tunaangalia mechi zijazo hatua ya robo fainali. Tunaamini tutapambana kufanya vizuri zaidi, “ amesema Fei Toto

    Kocha Mkuu wa Tanzania, Hemed Suleman ameweka wazi kuwa makosa yaliyopita watafanyia kazi ili kupata matokeo kwenye mechi zijazo.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleSIMBA SC KUZINDUA UZI MPYA AGOSTI 27 2025
    Next Article ISAK AVUNJA UKIMNYA, ADAI KUNA USALITI UMEFANYIKA

    Related Posts

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.