Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » SIMBA WABAKI NJIA PANDA, TAFSIRI TOFAUTI YA KAPOMBE
    KITAIFA

    SIMBA WABAKI NJIA PANDA, TAFSIRI TOFAUTI YA KAPOMBE

    ChikaoBy ChikaoFebruary 9, 202601 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    MAHODHA wa Simba, Shomari Kapombe aibua gumzo baada ya kushindwa kuweka wazi maana halisi ya staili yake mpya ya kushangilia mabao, inayohusisha kutembea kama mzee anayesaidiwa na mkongojo, akisema ni staili atakayoendelea nayo kila anapofunga.

    Kapombe alionekana kwa mara ya kwanza akitumia staili hiyo katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Esperance de Tunis, uliochezwa hivi karibuni, ambapo alishangilia kwa namna iliyowaacha wengi njia panda.

    Katika kushangilia huko, beki huyo wa kulia alionekana akishika mfano mkongojo, ishara iliyozua tafsiri tofauti miongoni mwa mashabiki, huku baadhi wakiamini ni ujumbe maalum aliokusudia kuuwasilisha.

    Akizungumza kuhusu staili hiyo, Kapombe amesema  ameamua kuitumia kama sehemu ya kujipa motisha binafsi, hasa kutokana na maneno ya kubezwa anayopata kutoka kwa baadhi ya watu.

    Nahodha huyo wa Simba aliongeza kuwa kila atakapopata nafasi ya kufunga, ataendelea kushangilia kwa staili hiyo ya kutembea kama mzee, kama njia ya kuwajibu wanaomdharau au kumuita mzee.

    “Hivi sasa nawaacha wanaoelewa maana yake waendelee kuelewa kwa njia yao, lakini hapo baadaye nitaweka wazi sababu hasa zilizonifanya nichague hii staili,” amesema  Kapombe.

    Kwa mujibu wa taarifa zilizopo, staili hiyo ya Kapombe inalenga kuwapa majibu wale wanaomkosoa na kumbeza, huku akionyesha kuwa bado ana nguvu, ari na ‘damu inayochemka’ ndani ya uwanja.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleMILIONI 500 KUWAPELEKA YANGA ROBO FAINALI
    Next Article Mbwana Samatta na Simon Msuva Hali Ngumu Huko Walipo, Hawatupii Tena

    Related Posts

    KOCHA WA YANGA HAELEWI, VIONGOZI WABADILISHA UELEKEO

    March 25, 2026

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    TETESI: TIMU YA MESSI YAMFUKUZIA BERNARDO SILVA

    KOCHA WA YANGA HAELEWI, VIONGOZI WABADILISHA UELEKEO

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.