Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home ยป Mbwana Samatta na Simon Msuva Hali Ngumu Huko Walipo, Hawatupii Tena
    KITAIFA

    Mbwana Samatta na Simon Msuva Hali Ngumu Huko Walipo, Hawatupii Tena

    ChikaoBy ChikaoFebruary 9, 202602 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    LICHA ya nyota wawili Mbwana Samatta na Simon Msuva kuwa na umuhimu mkubwa kwenye kikosi cha timu ya taifa, Taifa Stars takwimu zinaonyesha msimu huu bado hawajaonyesha viwango vikubwa wakiwa kwenye klabu wanazozitumikia.

    Katika mechi 13 alizocheza msimu huu wa Ligi Kuu Ufaransa, mshambuliaji huyo bado hajafunga bao wala kutoa asisti tofauti na msimu uliopita alipokuwa PAOK ya Ugiriki.

    Akiwa PAOK, Samatta alifunga mabao manne na kutoa asisti moja katika mechi 12, takwimu zilizothibitisha bado ana uwezo wa kumalizia nafasi.

    Hata hivyo, ni kama uhamisho wake wa kwenda Le Havre umeambatana na ugumu wa ligi, kasi ya mechi na majukumu ya kucheza nafasi tofauti za ushambuliaji.

    Samatta hatumiki kama mshambuliaji wa mwisho pekee mara nyingi hushuka chini kusaidia ujenzi wa mashambulizi, kufungua nafasi kwa wachezaji wa pembeni na kupambana na mabeki wenye nguvu.

    Hilo limeathiri idadi ya nafasi anazopata za kufunga, lakini halijafuta mchango wake kiufundi ndani ya timu.

    Ndiyo maana licha ya kutofunga mabao, benchi la ufundi la Le Havre limeendelea kumuamini, ishara kwamba nyota huyo anatoa zaidi ya kufunga.

    Download Gospel Songs: https://hizigospel.com/

    Kwa Simon Msuva naye hali si shwari kwani msimu huu amefunga mabao mawili na kutoa asisti nne katika mechi 12, tofauti na msimu uliopita alipofunga mabao 12 katika mechi 11.

    Takwimu zinaonyesha msimu huu ameshuka hasa katika kufumania nyavu za wapinzani tofauti na msimu uliopita ambao alikuwa na wastani wa kufunga bao moja kwa kila mechi.

    Hata hivyo, kubadilishiwa majukumu kwenye kikosi hicho imekuwa moja ya sababu ya nyota huyo kutoanza na makali akitumika zaidi kama mchezeshaji wa pembeni kuliko mshambuliaji.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleSIMBA WABAKI NJIA PANDA, TAFSIRI TOFAUTI YA KAPOMBE
    Next Article SIMBA WATIKISWA, YANGA WAPANGIA ROBO FAINALI

    Related Posts

    KOCHA WA YANGA HAELEWI, VIONGOZI WABADILISHA UELEKEO

    March 25, 2026

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    TETESI: TIMU YA MESSI YAMFUKUZIA BERNARDO SILVA

    KOCHA WA YANGA HAELEWI, VIONGOZI WABADILISHA UELEKEO

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.