VINARA wa Ligi Kuu ya England, Arsenal hawatanii kabisa msimu huu, wanaendelea kukusanya pointi kwenye kila mchezo wanaocheza na kuwakimbia wale wanaowafukuza ambao ni Manchester City.
Jana waliichabanga Sunderland 3-0 na kuongeza wigo wa pointi dhidi yake na City na sasa ubao unasoma tofauti ya pointi tisa huku Man City akiwa na mchezo mgumu leo dhidi ya Liverpool.
Kwa kasi waliyonayo msimu huu kuna kila dalili vijana hawa wa Mikel Arteta wakatwaa ubingwa wa EPL msimu.