Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » MBEYA DAY NI LEO KUNOGESHWA NA MECHI KALI DHIDI YA AZAM FC
    KITAIFA

    MBEYA DAY NI LEO KUNOGESHWA NA MECHI KALI DHIDI YA AZAM FC

    ChikaoBy ChikaoSeptember 6, 202502 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    PAZIA la Ligi Kuu Tanzania Bara ya NBC ambayo ni namba nne kwa ubora linakaribia kufunguliwa ikiwa ni siku zinahesabiki kwa kuwa Septemba 17 kazi inatarajiwa kuanza.

    Leo kuna tamasha kubwa nyanda za juu Kusini, ambapo Mbeya City iliyorejea kwa mara nyingine ndani ya Ligi Kuu Tanzania Bara ambayo ni namba nne kwa ubora Afrika watakuwa na jambo lao.

    Mbey City, The Purple Nation,  Uwanja wa Sokoine, Mbeya watafanya utambulisho wa kikosi chao cha msimu wa 2025/2026 unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.

    Miongoni mwa wachezaji waliopo Mbeya City ni kipa wa zamani wa Simba SC na Yanga SC, Beno Kakolanya ambaye yupo hapo kwa mara nyingine tena katika kutimiza majukumu yake.

    Kutakuwa na mchezo mkali wa kirafiki kati ya wenyeji Mbeya City dhidi ya matajiri wa Dar, Azam FC ambao unatarajiwa kuchezwa Uwanja wa Sokoine, Mbeya.

    Kocha Msaidizi wa Mbeya City Mussa Rashid ameweka wazi kuwa wapo tayari kwa mchezo huo na watatoa burudani nzuri kwa mashabiki watakaojitokeza.

    Hasheem Ibwe, Ofisa Habari wa Azam FC ameweka wazi kuwa wapo tayari kwa mchezo na wapinzani wao Mbeya City wamefanya makosa kuichagua Azam FC kwa kuwa ina hasira kutafuta matokeo hata kama imealikwa.

    Mgeni rasmi kwenye tamasha hilo ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Beno Malisa atashuhudia burudani zote kwenye tukio hili kubwa.

    Azam FC
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleMIKE TYSON KUZICHAPA NA FLOYD MAYWEATHER
    Next Article Barcelona, Liverpool na Madrid vitani kumgombea Marc Guehi

    Related Posts

    YANGA, AZAM FC USO KWA USO KUSAKA FAINALI YA MUUNGANO

    April 25, 2026

    SIMBA YASHIKA NAFASI YA 19 DUNIANI, IPO LEVO ZA MADRID

    April 25, 2026

    TAREHE PAMOJA NA UWANJA AMBAO DABI YA KARIAKOO ITAPIGWA

    April 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    YANGA, AZAM FC USO KWA USO KUSAKA FAINALI YA MUUNGANO

    SIMBA YASHIKA NAFASI YA 19 DUNIANI, IPO LEVO ZA MADRID

    HILI HAPA DAU LA KUMPATA COLE PALMER

    TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMAMOSI TAREHE 25.4.2025

    PRESHA YA KUUKOSA UBINGWA YATAWALA REAL MADRID

    TAREHE PAMOJA NA UWANJA AMBAO DABI YA KARIAKOO ITAPIGWA

    SIMBA SC YAWINDA MAJIBU KWA MLANDAGE, SI KISASI

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.