Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home ยป FADLU ATHIBITISHA KUONDOKA SIMBA, AWAAGA MASHABIKI KWA HESHIMA
    KITAIFA

    FADLU ATHIBITISHA KUONDOKA SIMBA, AWAAGA MASHABIKI KWA HESHIMA

    ChikaoBy ChikaoSeptember 22, 202501 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Fadlu
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    Baada ya kuagana rasmi na mabingwa wa kihistoria wa Tanzania, Simba SC, kocha raia wa Afrika Kusini Fadlu Davids sasa amejiunga na wakali wa Morocco, Raja Club Athletic, kama kocha mkuu.

    Kwa mujibu wa taarifa kutoka vyanzo vya karibu na klabu hiyo, makubaliano yote kati ya pande mbili yamekamilika, na Fadlu anarejea katika timu aliyowahi kuitumikia kama kocha msaidizi. Wakati huo, Raja walitwaa ubingwa wa Botola Pro bila kupoteza mchezo wowote msimu mzima, rekodi iliyowaweka kileleni barani Afrika.

    Kwa sasa, Davids yupo nchini Afrika Kusini na anatarajiwa kuondoka kesho kuelekea Morocco ili kuanza rasmi majukumu yake. Hatua hii inafungua ukurasa mpya wa maisha yake ya ukocha, safari ambayo safari hii anaingia kama kocha mkuu wa Raja Casablanca.

    Raja Club Athletic, moja ya vilabu vikongwe na vyenye mashabiki wengi barani Afrika, imepania kurejea katika nafasi ya juu zaidi, hasa kwenye mashindano ya CAF Champions League. Uongozi wa klabu hiyo umeahidi kumpa Fadlu na benchi lake la ufundi sapoti ya kutosha kuhakikisha ndoto hizo zinatimia.

    Kwa ujio wake, mashabiki wa Raja wanatarajia mwendelezo wa falsafa yake ya soka ya kushambulia kwa kasi na nidhamu ya kiufundi, huku wakiamini anaweza kurejea utukufu wa zamani wa klabu hiyo.

    Simba SC
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleFADLU SAFARI YA KUIACHA SIMBA, RASMI IMEWADIA, KUONDOKA KESHO
    Next Article SIMBA YATANGAZA RASMI UWANJA WA MKAPA KUWA UWANJA WAO WA NYUMBANI 2025/2026

    Related Posts

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.