Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, inatarajiwa kushuka dimbani usiku wa leo kuwakabili wenyeji wao, Bafana Bafana ya Afrika Kusini, katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa utakaopigwa kwenye Uwanja wa Peter Mokaba kuanzia saa 2:30 usiku kwa saa za Afrika Mashariki. Mchezo huu unatoa nafasi ya kutengeneza pesa kubwa kwa wabashiri kupitia Meridianbet.
Licha ya kuwa ni mchezo wa kirafiki, pande zote mbili zimeupokea kwa uzito mkubwa, zikilenga kuutumia kama sehemu ya maandalizi ya mashindano ya COSAFA yanayoendelea nchini Afrika Kusini. Kwa upande wa Tanzania, mchezo huu pia ni sehemu ya maandalizi kuelekea michuano ya CHAN inayotarajiwa kufanyika mwezi Agosti, sambamba na kujiandaa kwa mechi za kufuzu Kombe la Dunia zitakazopigwa mwezi Septemba mwaka huu. Weka mkeka wako kwenye mchezo huu pamoja na michezo mingine mingi sana inayopatikana Meridianbet.
Akizungumza na vyombo vya habari kabla ya mchezo huo, Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Hemed Suleiman ‘Morocco’, amesema kuwa mchezo dhidi ya Afrika Kusini ni fursa muhimu ya kuimarisha kikosi chake, huku pia akitumia nafasi hiyo kupima uwezo wa wachezaji wake.
NB: Jisajili na Meridianbet na cheza michezo ya kasino ya mtandaoni upate ushindi kirahisi, Pia ongeza maokoto yako kwa kubashiri michezo mbalimbali yenye ODDS KUBWA. PIGA *149*10# AU tembelea tovuti yao meridianbet.co.tz
Kikosi cha Taifa Stars kinajumuisha wachezaji waliopo kwenye ligi ya nyumbani pamoja na wanaocheza nje ya nchi, akiwemo Simon Msuva (Al Talaba – Iraq), Selemani Mwalimu (Wydad AC – Morocco), na Alphonce Mabula (Shamakhi – Azerbaijan). Wachezaji hawa wanatarajiwa kuongeza uzoefu wa kimataifa katika kikosi, hususan kuelekea mashindano ya CECAFA.
Rekodi ya kukutana kwa timu hizi inaonyesha wamekutana mara tatu na wote wameshinda mchezo mmoja mmoja na kutoa sare moja. Mwaka 2002 timu hizo zilitoka sare ya bao 1-1, kabla ya Afrika Kusini kushinda bao 1-0 mwaka 2011 katika mchezo wa kirafiki, na kisha Taifa Stars kushinda bao 1-0 katika michuano ya COSAFA ya mwaka 2017.
Mchezo wa leo unatarajiwa kuwa wa ushindani mkubwa na burudani ya aina yake, huku Taifa Stars ikisaka matokeo chanya na kuendeleza rekodi nzuri dhidi ya Bafana Bafana. Ushindani hautokuwa uwanjani pekee bali pia wale mabingwa wa kubashiri watakua wanausaka ushindi wao kupitia Meridianbet