Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » YANGA WANAMTAFUTA MWENYE KISU KIKALI KUMCHUKUA MZIZE
    KITAIFA

    YANGA WANAMTAFUTA MWENYE KISU KIKALI KUMCHUKUA MZIZE

    ChikaoBy ChikaoAugust 11, 202501 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Yanga
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    ….. OFA IMEKATALIWA. Jana tulilala na neno hili.

    Barua za Waarabu zimeendelea kupishana pale Jangwani. Inaingia barua hii, baada ya muda inaingia barua nyingine. Zote zinazungumzia upatikanaji wa Mzize.

    Wanachokifanya Yanga SC ni kumtafuta yule mwenye kisu kikali ndio ale nyama. Mimi siamini kama Mzize atacheza Yanga SC msimu ujao. Hili siamini, lakini wanachokifanya Yanga SC ni kuiongezea thamani biashara ya Mzize. Itafika tu timu ambayo itatoa ofa ya maana na itakuwa ngumu ofa hiyo kukataliwa. Uzuri Mzize mwenyewe anazidi kuichonganisha biashara yenyewe. Juzi ametupia mabao mawili katika jezi za Stars.

    Ninachoamini iko timu itafikia kiasi ambacho Yanga SC watakipokea. Rais wa Real Madrid Frolentino Perez aliwahi kuwaambia Juventus kuwa hakuna mchezaji asiyeuzwa baada ya kuulizia upatikanaji wa Zidane. Juve ndio walimjibu Perez kwa dharau kuwa Zidane hauzwi.

    Baada ya wiki moja Perez kutoa kauli ile, Uwanja wa Santiago Bernabeu ulijaa mashabiki waliokuja kutazama utambulisho wa Zidane. Perez alirudi Juve kikubwa na kutoa fedha ambazo Juve walishindwa kuzikataa. Biashara ya Yanga SC na Mzize itaenda kuisha katika namna hii ya Juve, Zidane na Madrid. Ni ngumu kushikilia bomba hadi mwisho.

    Ameandika @abdulmkeyenge1

    Yanga SC
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleHAYA HAPA MAGAZETI YA LEO TAREHE 11-08-2025
    Next Article SIMBA SC BADO IPO SOKONI

    Related Posts

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.