Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home ยป USAJILI WA KWANZA SIMBA HUU HAPA, MSHAMBULIAJI WA MABAO KUTAMBULISHWA
    KITAIFA

    USAJILI WA KWANZA SIMBA HUU HAPA, MSHAMBULIAJI WA MABAO KUTAMBULISHWA

    ChikaoBy ChikaoJuly 27, 202501 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    MSIMBAZI kumeanza kumechangamka kupitia usajili baada ya dirisha la usajili kufunguliwa huku wakiwa hajatangaza mchezaji hata mmoja mpya ambaye ameshasaini kandarasi Simba SC.

    Mabosi wa Singida Black Stars, wameeleza kuwa Jonathan Sowah ambaye ni mshambuliaji wao wameingia makubaliano ya kumuuza ndani ya Simba SC kwa makubaliano maalumu.

    Hivyo Sowah anakuwa nyota wa kwanza usajili wake kuwekwa wazi baada ya timu ya Simba SC kuwa kwenye sarakasi nyingi kutokana na wachezaji ambao walikuwa wanatajwa kuwa kwenye hesabu za Kocha Mkuu, Fadlu Davids kutambulishwa kwa timu pinzani ambayo ni Yanga SC.

    Miongoni mwa wachezaji ambao walikuwa wanatajwa kuwa kwenye hesabu za Simba SC wakatambulishwa Yanga SC ni kiungo Ballac Conte ambaye kasaini dili la miaka mitatu Jangwani.

    Imeelezwa Sowah anakuja kuchukua nafasi ya straika Lionel Ateba ambaye anatarajiwa kutimkia uarabuni. Imethibitishwa kuwa Simba walikamilisha dili la Sowah usiku wa kuamkia Jumatano Julai 16 2025.

    Ikumbukwe kwamba kwa msimu wa 2024/25 Sowah kwenye ligi ikiwa ni ingizo jipya katika dirisha dogo alifunga jumla ya mabao 13 akiwa na Singida Black Stars ambayo ilicheza fainali ya CRDB Federation Cup dhidi ya Yanga SC ikapishana na taji hilo.

    Simba SC
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleRASMI: SIMBA SC IMEFIKIA MAKUBALIANO NA FEISAL
    Next Article NYOTA WA FOUNTAIN GATE ALAMBA MKATABA WA MIAKA 17

    Related Posts

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.