Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026
    KIMATAIFA

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    ChikaoBy ChikaoMarch 24, 202601 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    Kiungo nyota wa zamani wa Ufaransa, Zinedine Zidane, amekubali rasmi kurithi mikoba ya Didier Deschamps kama Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya Ufaransa baada ya kumalizika kwa Kombe la Dunia la FIFA 2026.

    Kwa mujibu wa taarifa zilizothibitishwa, Zidane anatarajiwa kuchukua jukumu hilo mara baada ya michuano hiyo itakayofanyika katika mataifa ya Marekani, Mexico na Canada.

    Kocha wa sasa, Deschamps, amekuwa akiinoa Ufaransa tangu mwaka 2012, lakini tayari ameshaweka wazi kuwa ataachia ngazi baada ya Kombe la Dunia lijalo. Hatua hiyo itahitimisha safari yake ya miaka 14 yenye mafanikio makubwa akiwa na kikosi hicho.

    Katika kipindi chake, Deschamps aliiongoza Ufaransa kufika fainali ya UEFA Euro 2016 pamoja na fainali ya Kombe la Dunia la FIFA 2022 nchini Qatar.

    Uteuzi wa Zidane unatajwa kuwa mwanzo mpya kwa timu hiyo, huku mashabiki wengi wakitarajia kuona mafanikio zaidi chini ya nahodha huyo wa zamani aliyewahi kuipa Ufaransa heshima kubwa akiwa mchezaji.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleKatibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.
    Next Article Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Related Posts

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    March 20, 2026

    RICHARLISON SHUJAA WA TOTTENHAM VS LIVERPOOL, WAIPINGIZA MAKALI

    March 16, 2026

    WEST HARM WAISHIKILIA MAN CITY, MBIO ZA UBINGWA ZAPAMBA MOTO

    March 16, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.