West Ham United wamewalazimisha Manchester City kwa sare ya 1–1 katika mchezo wa Premier League uliokuwa na ushindani mkubwa.
City walitangulia kufunga kupitia Bernardo Silva dakika ya 31, lakini West Ham wakajibu haraka kupitia Konstantinos Mavropanos dakika ya 35, na kuifanya mechi hiyo kumalizika kwa sare.
Matokeo hayo yanamaanisha Arsenal F.C. sasa wako pointi 9 mbele kileleni mwa msimamo. Hata hivyo City bado wana mchezo mmoja mkononi na mchezo huo ni dhidi ya Arsenal wenyewe.
Hivyo basi, pambano hilo linaweza kuwa fainali ya kweli ya ubingwa, ambapo City watajaribu kupunguza pengo huku Arsenal wakitaka kufunga kabisa mbio za taji.
