Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home ยป RASMI AL NASR YAMCHOMOA KIBU DENIS MSIMBAZI KWA MILIONI 776
    KITAIFA

    RASMI AL NASR YAMCHOMOA KIBU DENIS MSIMBAZI KWA MILIONI 776

    ChikaoBy ChikaoFebruary 10, 202601 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    kibu denis
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    Al Nasr imefikia makubaliano rasmi na Simba ya kumnunua mshambuliaji Kibu Denis baada ya klabu hiyo ya Libya jana kukubaliana maslahi binafsi na nyota huyo wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’.

    Baada ya awali Simba kuonyesha utayari wa kumuuza Kibu Denis, kilichobakia kilikuwa ni makubaliano binafsi baina ya Al Nasr na Kibu Denis ambayo yalichelewa kufanyika kwa vile mchezaji huyo alikuwa Angola akiitumikia Simba katika mchezo wa raundi ya tano ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu huu.

    Lakini baada ya nyota huyo kurejea, jana, Jumatatu, Februari 9, 2026, miamba hiyo ya Libya ilikutana na upande wa mchezaji huyo na wakakubaliana rasmi na hivyo mchezaji huyo ataungana na Al Nasr.

    Uhamisho huo utaifanya Simba ivune kiasi cha Dola 300,000 (Sh776 milioni) kwa kukubali kumuachia Kibu ambaye mkataba wake ulibakia miezi mitano ufikie tamati.

    Msimamizi wa Kibu Denis, Carlos Sylivester amesema kuwa taarifa zozote kuhusu mshambuliaji huyo zitatolewa na Simba.

    Ndani ya Al Nasr, Kibu atakutana na nyota wawili aliocheza nao Simba hivi karibuni ambao ni kiungo Fabrice Ngoma na mshambuliaji Steven Mukwala pamoja na Aziz Ki anayecheza Al Ittihad.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleKOCHA WA SIMBA AICHIMBA MKWARA KMC FC
    Next Article Tanzania Yaiomba China Msaada Kukamilika Miundo Mbinu ya AFCON 2027

    Related Posts

    KOCHA WA YANGA HAELEWI, VIONGOZI WABADILISHA UELEKEO

    March 25, 2026

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    TETESI: TIMU YA MESSI YAMFUKUZIA BERNARDO SILVA

    KOCHA WA YANGA HAELEWI, VIONGOZI WABADILISHA UELEKEO

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.