Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home ยป Tanzania Yaiomba China Msaada Kukamilika Miundo Mbinu ya AFCON 2027
    KITAIFA

    Tanzania Yaiomba China Msaada Kukamilika Miundo Mbinu ya AFCON 2027

    ChikaoBy ChikaoFebruary 10, 202601 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Tanzania
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    Serikali ya Tanzania imeiomba Jamhuri ya Watu wa China kuunga mkono juhudi za Tanzania katika kuimarisha miundombinu ya kisasa ili kujiandaa vyema na uenyeji wa fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2027).

    Wito huo umetolewa hivi karibuni na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, James Millya, wakati wa hafla ya kusherehekea Mwaka Mpya wa China iliyofanyika katika Ubalozi wa nchi hiyo jijini Dar es Salaam.

    Millya amesisitiza kuwa maandalizi ya AFCON 2027 ni zaidi ya michezo, akiyataja mashindano hayo kama fursa ya kimkakati kwa ajili ya mabadiliko ya kiuchumi kwa kuchochea ukuaji wa uchumi kupitia biashara na utalii, upanuzi wa miundombinu ukihusisha ujenzi na ukarabati wa viwanja vinavyokidhi viwango vya kimataifa na kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania, nchi jirani za Afrika Mashariki na washirika wa kimataifa kama China.

    Naibu Waziri amebainisha kuwa uenyeji wa mashindano hayo unahitaji uwekezaji mkubwa katika mifumo ya usafirishaji, huduma za kijamii, na viwanja vya kisasa. China, ikiwa ni mshirika mkuu wa Tanzania katika ujenzi wa miundombinu mikubwa, inatajwa kuwa na mchango muhimu katika kufanikisha azma hiyo ya nchi za Afrika Mashariki.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleRASMI AL NASR YAMCHOMOA KIBU DENIS MSIMBAZI KWA MILIONI 776
    Next Article MO DEWJI AHOJI MAGEUZI SIMBA, GUMZO MTANDAONI

    Related Posts

    KOCHA WA YANGA HAELEWI, VIONGOZI WABADILISHA UELEKEO

    March 25, 2026

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    TETESI: TIMU YA MESSI YAMFUKUZIA BERNARDO SILVA

    KOCHA WA YANGA HAELEWI, VIONGOZI WABADILISHA UELEKEO

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.