HomeTETESI ZA SOKATETESI: MPANZU WA SIMBA SC KWENYE RADA ZA WAARABU

TETESI: MPANZU WA SIMBA SC KWENYE RADA ZA WAARABU

Mpanzu wa Simba kwenye Rada za Waarabu

INAELEZWA kuwa winga chaguo la kwanza la Kocha Mkuu, Fadlu Davids ndani ya kikosi cha Simba SC, Ellie Mpanzu yupo kwenye rada za RS Berkane,Waarabu wa Morocco.

Mpanzu ni miongoni mwa wachezaji waliokuwa tegemeo katika kikosi cha Simba SC msimu wa 2024/25 kwenye anga la kimataifa na kitaifa.

Ndani ya ligi rekodi zinaonyesha kuwa alicheza jumla ya mechi 17 kati ya 30. Ikumbukwe kwamba Mpanzu aliibuka ndani ya Simba SC kwenye dirisha dogo la usajili.

Simba SC ikiwa imefunga mabao 69 kahusika kwenye mabao 7, akifunga manne na kutoa pasi tatu. Ni dakika 1,239 alikomba uwanjani.

Ikiwa RS Berkane wataipata saini yake, Simba SC itakuwa na kazi kusaka winga mwingine ambaye atakuja katika kikosi hicho.

RELATED ARTICLES

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Most Popular

Recent Comments

Web Development Company in Kochi,Kerala on NEYMAR AMWAGA MACHOZI AKIKUTANA NA KIPIGO KIKUBWA ZAIDI KWAKE