Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home ยป NASIMAMA NA SIMBA NA AZAM WALIOCHAGUA KUKAA KIMNYA
    KITAIFA

    NASIMAMA NA SIMBA NA AZAM WALIOCHAGUA KUKAA KIMNYA

    ChikaoBy ChikaoAugust 19, 202502 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    “Nimeona andiko la kaka yangu Jemedari Said kuzihusu Simba SC na Azam FC kutokutoa matokeo yao ya mechi zao za kirafiki walizocheza.

    Azam FC walifungwa 2-1 na JKT Tanzania pale Arusha. Simba SC wakafungwa 4-3 na Enpipp pale Misri. Kwangu ni tofauti kidogo.

    Nasimama na Azam FC na Simba SC waliochagua kukaa kimya na taarifa za matokeo ya mechi zao. Kuna kitu kinaitwa mechi za Indoor. Hizi ni mechi ambazo hazina mashabiki. Hazitakiwi kutoka nje ndio maana zikaitwa Indoor.

    Makocha wanapenda kuzitumia mechi hizi kwa ajili ya kutazama mbinu zao zinafanyaje kazi. Timu zetu huwa zinacheza sana mechi zenye sura hii.

    Simba ambao walifungwa juzi, walicheza mechi nyingine na walishinda, lakini hawajapost matokeo ya mechi katika ukurasa wao na hata mtu mmoja aliyehoji.

    Hata waliotoa taarifa ya mechi ile ambayo Simba SC walishinda walipata shida kupata matokeo. Lakini hi haikuonekana kama ni shida.

    Kilionekana kitu cha kawaida tu. Kama Simba wangetoa matokeo ya mechi ile waliyoshinda, kisha hawajapost matokeo ya mechi ya juzi, ingeleta shida kwa wapenzi wao na moja kwa moja tungesema wanachagua taarifa za kuzitoa.

    Lakini walivyoshinda hawajatoa matokeo. Kwanini tuhoji walivyofungwa? Mimi naamini hizi ni mechi ambazo zipo sana na zinachezwa sana pale Avic Town. Bunju Arena. Chamazi. KMC Complex zinachezwa sana, tena kila siku au nyingine asubuhi na nyingine jioni. Ni mechi za kawaida mno. Ni kawaida sana.

    Binafsi nimewahi kushuhudia mechi zenye sura hii nyingi tu zilizokosa idadi. Tena nimetazama mechi za Simba SC na Yanga SC matokeo yake yanabaki ndani pale pale” Ameenda Mkunga

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleRAIS WA FIFA AMPONGEZA KARIA KWA KUREJEA TENA MADARAKANI
    Next Article PITIA MAGAZETI YA MICHEZO LEO TAREHE 20 AGOSTI 2025

    Related Posts

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.