Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » VILABU VYA TANZANIA VYAANZA NA MOTO MECHI ZA KIMATAIFA
    KIMATAIFA

    VILABU VYA TANZANIA VYAANZA NA MOTO MECHI ZA KIMATAIFA

    ChikaoBy ChikaoSeptember 21, 202501 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    tanzania
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    Katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL), Simba SC ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Gaborone United ya Botswana kwenye mchezo uliopigwa mjini Gaborone. Bao pekee la mchezo huo lilifungwa dakika ya 15 na Mpanzu, na kuwapa Wekundu wa Msimbazi faida kubwa kuelekea mchezo wa marudiano jijini Dar es Salaam.

    Kwa upande mwingine, kwenye Kombe la Shirikisho Afrika (CAFCC), Singida Black Stars walionyesha uimara wao baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Rayon Sports ya Rwanda. Bao la ushindi lilipachikwa wavuni na Serge Tchakei dakika ya 23 na kuiweka Singida katika nafasi nzuri ya kusonga mbele.

    Ushindi huo unakuja siku chache baada ya mabingwa wa Tanzania, Yanga SC, kuilaza Williete SC ya Angola kwenye mchezo wa kwanza wa Ligi ya Mabingwa Afrika, huku Azam FC nao wakipata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya El Merriekh Bentiu ya Sudan Kusini kwenye CAFCC.

    Kwa matokeo haya, vilabu vya Tanzania vimefanikiwa kusajili ushindi kwenye michezo yote minne ya wiki hii, jambo linaloleta matumaini makubwa kwa mashabiki na kuimarisha taswira ya soka la nchi hiyo katika ngazi ya kimataifa.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleMAJIBU KUHUSU USHINDI WA SIMBA UGENINI KUWA NI BAHATI
    Next Article Majina ya Waliochaguliwa Kusimamia Uchaguzi Temeke 2025

    Related Posts

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    March 24, 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    March 20, 2026

    RICHARLISON SHUJAA WA TOTTENHAM VS LIVERPOOL, WAIPINGIZA MAKALI

    March 16, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.