Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » SIMBA SC YATAJA HASARA WALIYOPATA KWENYE MCHEZO WA LEO
    KITAIFA

    SIMBA SC YATAJA HASARA WALIYOPATA KWENYE MCHEZO WA LEO

    ChikaoBy ChikaoSeptember 28, 202502 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    simba
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    UONGOZI wa Simba SC umebainisha hasara watakazopata kutokana na kuwakosa mashabiki kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Gaborone United ya Botswana, Septemba 28 2025 Uwanja wa Mkapa.

    Ahmed Ally, Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba SC amesema kuwa walipata adhabu kutokana na makosa ya mashabiki kwenye mechi zilizopita za kimataifa ikiwa ni mchezo wa Al Masry na RS Berkane.

    “Hasara ya kwanza tunakosa mashabiki, hasara ya pili tunakosa mapato na hasara ya tatu tunalipa faini ya USD 50,000. Vilevile tumepewa adhabu kutokana na mechi ya fainaili dhidi ya RS Berkane, huku vilevile tuliwasha fireworks. Kwenye mechi ya fainali tumetozwa faini ya USD 35,000. Jumla Tumetoshwa USD 85,000 sawa na Tsh. 200 milioni.

    “Tunacheza bila mashabiki kwenye mechi dhidi ya Gaborone United pekee lakini tumefanya makosa mfululizo CAF watakuwa makini na sisi kwelikweli sababu wanaona tunafanya vitendo ambavyo sio vya kiungwana hivyo watakuwa wanaangalia kama Simba Sports SC tumebadilika. Ni lazima tuwe makini kwelikweli ili kuwaonyesha kwamba tumejifunza na tumebadilika. Kuanzia hivi sasa tuchukue taswira mpya kwenye eneo la mashabiki.

    “Wapo mashabiki ambao wametaka kuwa sehemu ya maumivu ambayo tunapitia Klabu ya Simba na maumivu yenyewe ni faini ya Tsh. 212,500,000 sawa na USD 85,000. Kwa mapenzi yao mashabiki wameomba kuchangia faini ili kuipunguzia klabu mzigo na sisi tumepokea na tumeridhia mashabiki wachangie hususani kwenye eneo la faini,”.

    Leo Simba SC itakuwa na kazi kwenye anga la kimataifa katika Ligi ya Mabingwa Afrika, Uwanja wa Mkapa, saa 10:00 jioni.Mashabiki watakuwa Coco Beach ambapo hapo wataangalia mpira kwenye Big Screen.

    Post navigation

    Simba SC
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleSIMBU APANDISHWA CHEO JESHINI
    Next Article MWAMUZI WA TANZANIA KUONGOZA MICHEZO YA KOMBE LA DUNIA

    Related Posts

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.