Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » SIMBA IPO KAMILI KUWAVAA GABORONE LEO, MECHI YA KIMATAIFA
    KITAIFA

    SIMBA IPO KAMILI KUWAVAA GABORONE LEO, MECHI YA KIMATAIFA

    ChikaoBy ChikaoSeptember 20, 202501 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    simba
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    SEPTEMBA 20 2025 ni Gaborone United vs Simba SC mchezo wa hatua ya awali Ligi ya Mabingwa Afrika ambapo wababe hawa watakuwa katika dakika 90 za kusaka ushindi kabla ya mchezo wa pili utakaotoa mshindi wa jumla atakayekwenda hatua inayofuata.

    Fadlu Davids, Kocha Mkuu wa Simba SC amesema wanachohitaji ni ushindi ili kutimiza malengo ya kwenda hatua ya makundi.

    “Ili upate nafasi ya kwenda hatua ya makundi ambacho kinahitajika ni ushindi. Mechi zote iwe ugenini na nyumbani ni muhimu kushinda na sisi tumejiandaa kufanya hivyo.

    “Timu yangu imecheza mechi mbili zenye uzito mkubwa Simba Day na Ngao ya Jamii kwa hiyo imetuongezea ubora.

    “Hata hivyo namuheshimu sana kocha wa timu pinzani naiheshimu hii timu kwa sababu wao ni mabingwa,”.

    Simba SC itakuwa Uwanja wa Francistown ikiwa ni hatua ya awali Ligi ya Mabingwa Afrika saa 2:00 usiku kwa saa za Afrika Mashariki.

    Miongoni mwa wachezaji waliopo Botswana ni Ellie Mpanzu, Mousa Camara, Kibu Dennis, Joshua Mutale na Wilson Nangu. Miongoni mwa wachezaji ambao wataukosa mchezo wa leo ni Hamza ambaye ni beki alipata maumivu kwenye mchezo dhidi ya Yanga SC na Mohamed ambaye huyu alisajiliwa akiwa na majeraha bado hajawa imara.

    Simba SC
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleYANGA YAPATA USHINDI WAKE WA KWANZA KIMATAIFA
    Next Article HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO SEPTEMBA 21 2025

    Related Posts

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.