Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home ยป SIMBA SC YAMALIZANA NA BEKI MJESHI, KIPA WA CHAN
    KITAIFA

    SIMBA SC YAMALIZANA NA BEKI MJESHI, KIPA WA CHAN

    ChikaoBy ChikaoAugust 29, 202502 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    INATAJWA kuwa Simba SC imefanikiwa kumsajili beki wa kati wa Timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars na Klabu ya JKT Tanzania, Wilson Nangu kwa mkataba wa miaka miwili.

    Hivyo beki huyo aliyekuwa anatajwa kuwa kwenye rada za Yanga SC huenda msimu mpya wa 2025/26 akawa kwenye uzi wa Simba SC.

    Nangu amekuwa bora kwenye timu ya JKT Tanzania kwenye eneo la ulinzi jambo ambalo linatajwa kuwa sababuu ya Simba SC kuisaka saini yake kwa ajili ya kuwa naye kikosini.

    Kikosi cha Simba SC kilikuwa kambini Misri tayari Agosti 29 kimerejea kwenye ardhi ya Tanzania kwa maandalizi ya mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara inayotarajiwa kuanza Septemba 17 2025.

    Mbali na ligi kuna Simba Day ambayo inatarajiwa kuwa Septemba 10 2025 ambapo kutakuwa na mchezo wa kirafiki dhidi ya Gor Mahia ya Kenya.

    Kwa mujibu wa chanzo cha habari kutoka ndani ya Simba, JKT Tanzania imekubali kumuachia nyota kwa sharti la kupewa beki David Kameta na Awesu Awesu kwa mkopo wa mwaka mmoja.

    Mbali na Nangu inatajwa kuwa tayari Simba SC imemalizana na kipa namba moja wa JKT Tanzania ambaye alikuwa chaguo la kwanza kwenye mashindano ya CHAN 2024 na timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars Yakoub Seleman ambaye tayari ameshaagwa na timu yake hiyo.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleMSIMU MPYA WA LIGI KUU BARA KUANZIA SEPTEMBA 17, RATIBA IPO HAPA
    Next Article DABI YA KARIAKOO KUCHEZWA DECEMBER 13

    Related Posts

    KOCHA WA YANGA HAELEWI, VIONGOZI WABADILISHA UELEKEO

    March 25, 2026

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    TETESI: TIMU YA MESSI YAMFUKUZIA BERNARDO SILVA

    KOCHA WA YANGA HAELEWI, VIONGOZI WABADILISHA UELEKEO

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.