Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » PRESHA YA KUUKOSA UBINGWA YATAWALA REAL MADRID
    KIMATAIFA

    PRESHA YA KUUKOSA UBINGWA YATAWALA REAL MADRID

    ChikaoBy ChikaoApril 25, 202601 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    madrid
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    Mambo yamezidi kuwa magumu kwa Real Madrid katika mbio za kuwania ubingwa wa La Liga, baada ya kupoteza alama muhimu kufuatia sare ya 1-1 dhidi ya Real Betis ugenini, katika dimba la La Cartuja jijini Sevilla.

    Real Madrid walianza vyema mchezo huo, wakitangulia kupata bao kupitia Vinicius Junior mapema katika kipindi cha kwanza, bao lililoashiria matumaini ya kuondoka na pointi tatu muhimu.

    Hata hivyo, matumaini hayo yalififia katika dakika za mwisho kabisa za mchezo, pale Hector Bellerin alipofunga bao la kusawazisha kwa upande wa Real Betis katika dakika za nyongeza.

    Matokeo hayo yanaifanya Real Madrid kubaki nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi, wakiwa nyuma kwa alama nane dhidi ya vinara Barcelona, ambao bado wana mchezo mmoja mkononi. Hali hii inaongeza presha kubwa kwa Madrid, ambao sasa wanahitaji ushindi mfululizo huku wakitegemea wapinzani wao kudondosha alama ili kufufua matumaini ya ubingwa.

    Kwa sasa, mbio za ubingwa zinaonekana kuwa ngumu zaidi kwa Real Madrid, huku Barcelona wakionekana kuwa na kasi na uthabiti wa kuwapeleka karibu zaidi na taji hilo.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleTAREHE PAMOJA NA UWANJA AMBAO DABI YA KARIAKOO ITAPIGWA
    Next Article TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMAMOSI TAREHE 25.4.2025

    Related Posts

    HILI HAPA DAU LA KUMPATA COLE PALMER

    April 25, 2026

    REFA ATUMIA SIMU KAMA VAR

    April 17, 2026

    BERNARDO AAGWA NA MAN CITY RASMI

    April 16, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    YANGA, AZAM FC USO KWA USO KUSAKA FAINALI YA MUUNGANO

    SIMBA YASHIKA NAFASI YA 19 DUNIANI, IPO LEVO ZA MADRID

    HILI HAPA DAU LA KUMPATA COLE PALMER

    TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMAMOSI TAREHE 25.4.2025

    PRESHA YA KUUKOSA UBINGWA YATAWALA REAL MADRID

    TAREHE PAMOJA NA UWANJA AMBAO DABI YA KARIAKOO ITAPIGWA

    SIMBA SC YAWINDA MAJIBU KWA MLANDAGE, SI KISASI

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.