Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA
    KITAIFA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    ChikaoBy ChikaoMarch 24, 202601 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    UONGOZI wa klabu ya Simba umeweka wazi kuwa uamuzi wa kumuongezea mkataba kiungo Elie Mpanzu umetokana na tathmini ya kina ya benchi la ufundi, iliyothibitisha umuhimu wake kuendelea kusalia kikosini kwa msimu ujao.

    Benchi hilo la ufundi, linaloongozwa na Kocha Mkuu Steve Barker, liliridhishwa na mchango wa mchezaji huyo na kupendekeza aongezewe mkataba wa kuendelea kuitumikia timu hiyo kwa misimu miwili zaidi.

    Kutokana na mapendekezo hayo, Mpanzu amesaini mkataba mpya wa miaka miwili utakaomuweka ndani ya Simba hadi mwaka 2028, baada ya ule wa awali kufikia ukingoni.

    Akizungumza kuhusu suala hilo, Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally, amesisitiza kuwa kuongeza mkataba wa mchezaji huyo hakukutokana na presha ya ushindani kutoka kwa wapinzani wao, bali ni maamuzi ya kiufundi yaliyofanywa kwa maslahi ya timu.

    Alibainisha kuwa licha ya kuwapo kwa jitihada kutoka kwa wapinzani wao wakuu kumshawishi nyota huyo, Mpanzu aliamua kubaki Simba baada ya kuridhishwa na mwelekeo wa klabu hiyo.

    “Mapendekezo ya benchi la ufundi yalituongoza kufanya maamuzi haya. Tulimuita mchezaji, tukazungumza naye na hatimaye akakubali kuendelea kubaki ndani ya Simba,” amesema Ahmed.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleDIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA
    Next Article HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    Related Posts

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    March 24, 2026

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.