Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » MANGUNGU: MABADILIKO YA BENCHI LA UFUNDI NDIO YALIIVURUGA SIMBA
    KITAIFA

    MANGUNGU: MABADILIKO YA BENCHI LA UFUNDI NDIO YALIIVURUGA SIMBA

    ChikaoBy ChikaoFebruary 5, 202602 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    mangungu
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    MWENYEKITI wa Klabu ya Simba, Murtaza Mangungu, amesema mabadiliko ya ghafla katika benchi la ufundi yamechangia kwa kiasi kikubwa kutokuwa na mwanzo mzuri wa msimu huu kwa timu hiyo.

    Mangungu amesema msimu uliopita Simba ilikuwa chini ya kocha mpya, Fadlu Davids, ambaye alihitaji aina maalumu ya wachezaji watakaokwenda sambamba na falsafa yake ya soka, jambo lililowasaidia kumaliza msimu katika nafasi ya pili na kufika fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

    Ameeleza kuwa walipoanza msimu huu, uongozi uliingia sokoni kusajili wachezaji kulingana na mapendekezo ya kocha huyo, lakini ujio wa ofa kubwa kwa Davids uliwalazimu kumuacha aondoke, hali iliyovuruga mipango yao mapema.

    “Wakati tunaanza msimu na kusajili wachezaji aliowapendekeza, ikaja ofa kubwa kwake na hatukuwa na budi kumzuia. Hilo lilituvuruga sana kwa sababu tulilazimika kuingia sokoni tena kutafuta kocha mwingine,” amesema Mangungu.

    Ameongeza kuwa Simba ilifanikiwa kumpata Steve Barker, ambaye naye amekuja na falsafa yake ya uchezaji, hivyo kulikuwa na ulazima wa kufanya usajili mwingine wa wachezaji watakaosaidia timu kufikia malengo yake.

    Mangungu amesema ujio wa kocha mpya katikati ya mashindano, pamoja na usajili wa wachezaji wapya, bado ni changamoto kwa timu kutokana na kukosekana kwa muunganiko wa pamoja.

    Amefafanua kuwa mafanikio ya timu si juhudi zake peke yake bali ni matokeo ya ushirikiano wa viongozi wengine, hata hivyo lawama nyingi hutupwa kwake pale timu inapofanya vibaya.

    “Jambo ninalokubaliana nalo ni waache wapewe sifa wanaowapenda, lakini lawama zije kwangu. Mimi siwezi kufanya timu ifanye vibaya kwa makusudi, kwa sababu tumeunda bodi na menejimenti yenye uwezo wa kufanya kazi na benchi la ufundi au wachezaji,” amesema.

    Ameongeza kuwa kulingana na mgawanyo wa majukumu, yeye binafsi hana nafasi ya kukutana moja kwa moja na wachezaji, bali bodi hukaa na kuwasilisha maelekezo kwa menejimenti ili yawafikie wachezaji.

    Mangungu amesema kelele na vurugu zinazoshuhudiwa hazichochewi na mashabiki au wanachama wa kweli wa Simba, bali ni watu wachache walioundwa kwa ajili ya propaganda na kuiondoa klabu hiyo kwenye mstari wake.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleSALUM MAYANGA AKALIA KUTI KAVU MASHUJAA
    Next Article MMILIKI WA MBEYA KWANZA APIGA MKWARA HUU MZITO

    Related Posts

    KOCHA WA YANGA HAELEWI, VIONGOZI WABADILISHA UELEKEO

    March 25, 2026

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    TETESI: TIMU YA MESSI YAMFUKUZIA BERNARDO SILVA

    KOCHA WA YANGA HAELEWI, VIONGOZI WABADILISHA UELEKEO

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.