Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » KWA MARA YA KWANZA MOROCCO YAANDIKA HISTORIA YA KUSSHINDA KOMBE LA DUNIA KWA VIJANA
    KIMATAIFA

    KWA MARA YA KWANZA MOROCCO YAANDIKA HISTORIA YA KUSSHINDA KOMBE LA DUNIA KWA VIJANA

    ChikaoBy ChikaoOctober 21, 202501 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Morocco
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    Timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20 ya Morocco imeandika historia baada ya kutwaa taji la Kombe la Dunia la Vijana (FIFA U-20 World Cup) kwa mara ya kwanza, ikipata ushindi wa mabao 2–0 dhidi ya Argentina katika mchezo wa fainali uliopigwa Jumapili.

    Shujaa wa pambano hilo alikuwa mshambuliaji Yassir Zabiri, aliyetikisa nyavu mara mbili katika dakika ya 12 na 29, akiiongoza Morocco kutwaa ubingwa huo wa kihistoria. Ushindi huo umeifanya Morocco kuwa taifa la kwanza kutoka Afrika kushinda taji hilo tangu Ghana ilipofanikiwa mwaka 2009.

    Argentina, ambayo ilikuwa haijapoteza mchezo wowote hadi kufika fainali, ilikosa huduma ya nyota wake wawili muhimu Claudio Echeverri wa Bayer 04 Leverkusen na Franco Mastantuono wa Real Madrid CF — hali iliyochangia kuporomoka kwao katika mchezo wa mwisho.

    Safari ya Morocco kuelekea ubingwa ilikuwa ya kuvutia. Walimaliza hatua ya makundi wakiwa vinara baada ya kushinda dhidi ya Uhispania, Brazil na Mexico, kisha kuiondosha Korea Kusini katika hatua ya 16 bora, Marekani robo fainali, na Ufaransa nusu fainali kabla ya kuhitimisha kazi kwa kuivunja Argentina katika fainali.

    Post navigation

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleAZAM FC YAJAWA MATUMAINI YA KUBADILISHA HISTORIA YA KIMATAIFA
    Next Article Ronaldo kumsogeza Lewandowski Al-Nassr

    Related Posts

    HILI HAPA DAU LA KUMPATA COLE PALMER

    April 25, 2026

    PRESHA YA KUUKOSA UBINGWA YATAWALA REAL MADRID

    April 25, 2026

    REFA ATUMIA SIMU KAMA VAR

    April 17, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    matokeo ya Azam FC vs Yanga SC Leo 25/04/2026

    YANGA, AZAM FC USO KWA USO KUSAKA FAINALI YA MUUNGANO

    SIMBA YASHIKA NAFASI YA 19 DUNIANI, IPO LEVO ZA MADRID

    HILI HAPA DAU LA KUMPATA COLE PALMER

    TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMAMOSI TAREHE 25.4.2025

    PRESHA YA KUUKOSA UBINGWA YATAWALA REAL MADRID

    TAREHE PAMOJA NA UWANJA AMBAO DABI YA KARIAKOO ITAPIGWA

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.