Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » SIMBA YAENDELEZA KAMPENI YA KUTOKOMEZA JEZI FEKI
    KITAIFA

    SIMBA YAENDELEZA KAMPENI YA KUTOKOMEZA JEZI FEKI

    ChikaoBy ChikaoOctober 12, 202501 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    KAMPENI ya Simba SC ambayo ina lengo la kutokomeza jezi feki inaendelea ambapo Wananchi wamezidi kupewa elimu kuhusu faida za kununua jezi Original.

    Ahmed Ally, Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba SC ameweka wazi kuwa kununua jezi Original ni jambo ambalo kila Mtanzania anapaswa kujivunia.

    Oktoba 9 uongozi wa Simba SC uliweka kambi Mwanza na kutembelea baadhi ya vituo na kuzungumza na Wananchi wa Buhongwa, Nyegezi, Nyamagana, Kisesa na Machinjioni.

    Ahmed Ally amesema kuwa kununua jezi feki kunadumaza ustawi wa maendeleo kwa muwekezaji, timu na taifa kiujumla hivyo ni muhimu kununua jezi orijino ambazo zipo kwenye maduka maalumu.

    “Hii vita sio nyepesi kila mtu anatafuta njia yake kwenye utafutaji lakini kwa kupitia jezi feki kunaumiza vibaya mno ni hasara kwa muwekezaji, hasara kwa taifa kwa kuwa kuna kodi inakosekana na mapato yanapungua.

    “Wanaonunua jezi feki ni wengi lakini pengine inatokea ananunua bila kujua ila kwa sasa ni muhimu kila Mtanzania akafurahia kuvaa kitu orijino hiyo itakuwa ni faida kwake kwa kuwa ameichangia timu yake aipendayo na amechangia kulipa kodi na anachangia maendeleo ya timu.

    Simba SC
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleTFF YASIMAMISHA WACHEZAJI YANGA PRINCESS, KUPISHA UCHUNGUZI WA JINSIA
    Next Article SIMBA YAKATAA UHUNI KWENI KWENYE MPIRA WA MIGUU

    Related Posts

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.