Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home ยป TFF YASIMAMISHA WACHEZAJI YANGA PRINCESS, KUPISHA UCHUNGUZI WA JINSIA
    KITAIFA

    TFF YASIMAMISHA WACHEZAJI YANGA PRINCESS, KUPISHA UCHUNGUZI WA JINSIA

    ChikaoBy ChikaoOctober 8, 202501 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limesimamisha kwa muda mchezaji wa klabu ya Yanga Queens, Princess Jeanine Mukandiyisenga, raia wa Rwanda, kupisha uchunguzi wa kina kuhusu jinsia yake.

    Hatua hii imekuja baada ya sintofahamu kuibuka mitandaoni na katika baadhi ya duru za michezo, ambapo mashabiki na wadau wameanza kuhoji hali halisi ya jinsia ya mchezaji huyo, ambaye amekuwa akionesha kiwango cha juu mno katika michezo ya Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania.

    Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya TFF, uchunguzi huo unalenga kuthibitisha ukweli bila upendeleo, kwa mujibu wa kanuni za shirikisho hilo na taratibu za Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) kuhusu wachezaji wa kike.

    Kwa sasa, Mukandiyisenga atabaki nje ya kikosi cha Yanga Queens hadi uchunguzi utakapokamilika na matokeo rasmi kutolewa.

    TFF imewataka mashabiki na wadau wote wa soka kuwa watulivu na kuepuka kutoa maoni ya kudhalilisha au ya kibaguzi, ikisisitiza kuwa mchakato huu ni wa kawaida na wa kisheria katika michezo ya kimataifa.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleHAYA HAPA MAGAZETI YA LEO OKTOBA 8, 2025
    Next Article SIMBA YAENDELEZA KAMPENI YA KUTOKOMEZA JEZI FEKI

    Related Posts

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.