Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home ยป WACHEZAJI WAWILI SIMBA KUUKOSA MCHEZO NA NAMUNGO
    KITAIFA

    WACHEZAJI WAWILI SIMBA KUUKOSA MCHEZO NA NAMUNGO

    ChikaoBy ChikaoOctober 1, 202501 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    WAKIWA kwenye hesabu za kumtafuta kocha mpya, Msimbazi wataendelea kukosa huduma ya wachezaji wawili kwenye mchezo wa leo Oktoba Mosi 2025 Uwanja wa Mkapa dhidi ya Namungo.

    Simba SC kwa sasa ipo chini ya kocha msaidizi Suleman Matola ambaye atakiongoza kikosi hicho kwenye mchezo dhidi ya Namungo FC.

    Katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Gaborone United, Simba SC ilikuwa chini ya Kocha Mkuu Hemed Morocco ambaye alikuwa hapo kwa muda maalumu kwa mchezo huo.

    Hayo yote yalitokana na Fadlu Davids ambaye alikuwa na timu nchini Misri kwenye kambi kupata dili katika timu nyingine ambayo ni Raja Casablanca ya Morocoo.

    Kuelekea kwenye mchezo wa leo Uwanja wa Mkapa wachezaji wawili wa Simba SC hawapo kwenye mpango wa mchezo ambao ni Abdoulazack Hamza na kiungo mshambuliaji, Mohamed Bajaber kutokana na majeraha.

    Bajaber tangu amejiunga na Simba msimu huu akitokea Polisi Kenya, hakufanikiwa kucheza mchezo wowote wa mashindano kutokana na majeraha ya nyama za paja aliyoyapata kambini nchini Misri.

    Kwa mujibu wa kocha msaidizi wat imu hiyo, Selemani Matola nyota hao hawatakuwepo katika mipango yake ya mchezo wa kesho kutokana na majeraha, hivi sasa wanaendelea na matibabu kuhakikisha wanarejea haraka.

    Simba SC
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleMsimamo wa Ligi kuu NBC Tanzania 2025/2026
    Next Article TETESI: SIMBA YAMTAKA KOCHA WA ZAMANI WA YANGA

    Related Posts

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.